Na Oscar Assenga,TANGA.

RAIS Samia Suluhu anatarajiwa kuwasili kesho mkoani Tanga kwa ajili ya ziara ya siku mbili mkoani Tanga ambapo akiwa mkoani hapa  atazindua Chuo cha Jeshi la Uhamiaji cha Taifa.

Akizungumza leo wakati wa halfa ya kukabidhiwa ofisi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Omari Mgumba alisema Rais Samia ataingia mkoani Tanga mchana na atafanya ziara wilayani Mkinga

Mgumba alisema Rais Samia atazindua chuo hicho cha Jeshi la Uhamiaji kilichojengwa eneo la Kichaka Miba wilayani Mkinga ikiwemo kufunga mafumzo ya wanajeshi wa jeshi jipya la Uhamiaji zaidi ya 818 waliohitimu mafunzo.

Alisema baada ya Rais Samia ataondoka ambapo pia alitoa rai kwa wananchi wa mkoa huo kujitokeza kwa wingi kumlaki katika maeneo yote atayopita.

Mwisho.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: