Na Thobias Mwanakatwe
MBUNGE wa Jimbo la Songwe, Philip Mulugo, ameahidi kutoa Sh.milioni tatu
kwa ajili ya kununulia injini ya boti ili kuwasaidia wavuvi wa Kijiji cha
Iyovyo wanaovua samaki Ziwa Rukwa.
Akizungumza na wananchi wa kijiji hicho katika mwendelezo wa ziara yake ya
kuhamasisha maendeleo jimboni mwake,
alisema atatoa fedha hizo mwezi Oktoba mwaka huu na kuwataka wavuvi nao
waanze kuchonga mtubwi.
Mulugo aliwataka wavuvi ili waweze kupata mikopo zaidi inayotolewa na
halmashauri pamoja na Benki ya NMB wajiunge katika vikundi ili waweze
kutambulika na hivyo kuwa rahisi kukopesheka.
"Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ameruhusu mapato ya ndani ya
halmashauri ya asilimia 10 yatumike kukopesha vikundi vya akiba mama na vijana,
na pia benki ya NMB inakopesha vikundi na dhamana inakuwa ni kazi
mnayoifanya," alisema Mulugo..
Mulugo ambaye amekuwa akitimiza ahadi anazotoa kwa wakati, alisema wavuvi hao watakapojiunga katika vikundi atasimamia kuhakikisha wanapata mkopo wa fedha ambazo zitawawezesha kununulia boti ya kuvulia samaki.
Post A Comment: