Na Ahmed Mahmoud Waziri wa Kilimo Husein Bashe anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika maonesho ya kimataifa ya kilimo TanzFood Expro 2022 yenye kibwagiz mbiu Ladha ya Tanzania. Akizungumza na waandishi wa habari katika makao makuu ya EAC Jijini Arusha Mkurugenzi wa sekta ya uzalishaji ndani ya Jumuiya ya Afrika masharika Jean Baptiste amesema maonyesho hayo yatafanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 11 hadi 13 Amesema kwa siku tatu watatumia kujenga mtandao wa kibiashara katika mazingira ya kitaalamu na kwamba sekta hii ya kilimo sio kwa ajili ya Tanzania Pekee ndio maana kama Eac na KiliFair Promotion tumeungana ili nchi wanachama wa jumuiya ya Afrika mashariki tutoke na bidhaa zilizo bora. "Bidhaa bora zinahitajika sana ili kuweza kutangaza katika maonyesho haya kutoka kote katika jumuiya itasaidia kuongeza tija ya kuzalisha bidhaa zenye ubora wa kimataifa" Awali Mkrugenzi wa Kilifair Dominic Shoo Alisema kuwa maonesho ya kilimo TanzFood pia yatazinduliwa na Balozi wa Ujerumani nchini Regine Hess na Waziri wa Kilimo Husein Bashe na kuyaleta pamoja makampuni 120 ya hapa nchini na nchi za Eac. Alisema kuwa wanayofuraha kuona waonyeshaji wa ndani na nje ya nchi kutoka masoko mengine kuja kuangalia bidhaa zetu huku akiyataka makampuni ya mbegu na Mashine za kilimo kuleta bidhaa zao katika maonyesho. Kwa Upande wake Mkurugenzi Mwenza wa Kilifair Tom Kunkler alisema kuwa maonesho hayo washiriki watapata fursa ya kupata mafunzo ya kilimo na uzalishaji wa bidhaa ili waweze kushindana katika soko la kimataifa. Alisema kuwa mafunzo hayo kwa wakulima yatawasaidia kuongeza ubora na maendeleo katika sekta ya kilimo ambapo kauli mbiu yake ni Ladha ya Tanzania.
Share To:

Arusha Newsroom

Post A Comment: