Kaimu Meneja Msaidizi wa Forodha wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Mara Bw. Robert Busumabu akichangia hoja wakati wa semina kuhusu taratibu za forodha zinazotumika kuwahudumia wafanyabiashara wa kati na wadogo wanaotumia Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Semina hiyo imefanyika kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.

Afisa Msimamizi Mkuu wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Edwin Iwato akitoa elimu ya taratibu za forodha zinazotumika kuwahudumia wafanyabiashara wa kati na wadogo wanaotumia Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Elimu hiyo imetolewa kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.

Afisa Msimamizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Lameck Ndinda akitoa mafunzo ya huduma bora kwa wateja kwa watumishi wanaofanya kazi katika Kituo cha Huduma kwa Pamoja Mpakani Sirari. Mafunzo hayo yametolewa kufuatia kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea mkoani Mara.

Afisa Uhusiano kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bi Salome Mwandalanga akimsikiliza kwa makini mfanyabiashara wa Sirari Bw. Joseph Mokare wakati wa kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea katika Wilaya ya Tarime mkoani Mara.

Afisa Msimamizi wa Kodi kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Abdallah Seif akitoa elimu ya kodi kwa mfanyabiashara wa Sirari Bw. Jumanne Omari wakati wa kampeni ya elimu kwa mlipakodi mlango kwa mlango inayoendelea katika Wilaya ya Tarime mkoani Mara. (PICHA ZOTE NA TRA).
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: