Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga Kalisti Lazaro ametoa wito Kwa viongozi wa Dini kuendelea  kuhamasisha waumini na Jamii Kwa ujumla umuhimu wa kuhifadhi  na kuyalinda mazingira.


Wito huo ameutoa katika mkutano wa 49 wa kuwajengea  mahusiano mema kati ya Dini za Kiyahudi,Kikristo na Kiislamu pamoja na kuangazia Dini na mabadiliko ya tabiachi uliofanyika  Wilayani Lushoto.

  

Mkuu huyo wa Wilaya alisema kuwa  Kwa kufanya hivyo ni kutimiza  matakwa ya Sheria  ya usimamizi wa mazingira ya mwaka 2004 ambayo  imeweka wazi. Misingi ya jumla katika suala Zima  la uhifadhi  wa mazingira.


Mkuu wa Wilaya huyo amesema kuwa viongozi  wa Dini wanaowajibu  wa kuhakikisha  wanaendelea  kutoa elimu kupitia mafundisho  ya dini Juu ya kutimiza  matakwa  ya sera  ya mazingira  ya mwaka 2021 ili malengo yaliyowekwa na serikali katika sekta ya uhifadhi mazingira yanatimia na Tanzania  inakuwa mstari wa  mbele  katika kukabiliana  na mabadiliko ya tabiachi.


" Umefika wakati wa kutumia ndimi ,elimu  katika kuwaeleza  wafuasi  kuhusu athari  hasi za kimazingira  ili kulinda  Dunia na viumbe  vilivyopo ndani yake.


Alieleza kuwa  ardhi ni amana kutoka Kwa Mungu , binadamu ni wasimamizi hivyo Jamii inatakiwa  iishi Kwa kuthamini,kulinda  na Kutunza mazingira  Kwa kujiepusha  na uharibifu  wa aina yoyote ,ikiwemo  uchafuzi  wa mazingira na  uharibifu wa vyanzo vya maji.


Aidha alisisitiza kupitia mkutano huo ni lazima washiriki wapate msukumo kutoka kwenye mafundisho Kwa kuzidisha ari  ya kuishi katika kijani kibichi, kulinda na kuhifadhi mazingira huku wakiendelea kuimarisha maelewano baina yao na ulimwengu.


Katika kusisitiza utunzaji wa mazingira Alisema kuwa wao kama Wilaya wanatarajia kuanzisha kampeni ya upandaji miti ambapo kila kata itatakiwa kupanda miti laki moja.


Kwa upande wake Askofu wa Kanisa la KKT Dk Msafiri Mbulu Alisema kuwa  mkutano huo wa 49 umewashirikisha  viongozi wa Dini kutoka Tanzania na Zanzibar.

Share To:

Post A Comment: