Na. Angela Msimbira TAMISEMI


Waziri  wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Innocent Bashungwa  leo amekabidhiwa rasmi Ofisi na aliyekuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu ambaye . 


Makabidhiano hayo yamefanyika katika Ofisi ya  Rais - TAMISEMI iliyopo  Sokoine Jijijini  Dodoma ambapo Waziri  Ummy  ameishukuru Menejimenti na watumishi kwa ushirikiano walioonyesha  kipindi alipokuwa akihudumu katika ofisi hiyo.


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Inoncent Bashungwa amesema kuwa TAMISEMI si ngumu kama watumishi  wote watajenga  mahusiano bora  na kuhakikisha wanatimiza majukumu yao kwa wakati, na kuhakikisha wanatatua changamoto za wananchi  kwa kutoa huduma bora.


Waziri Bashungwa amewaagiza watumishi  wa Mamlaka za Serikali za Mitaa  kuhakikisha kuendelea kushirikiana katika kufanyakazi kwa umoja na mshikamano  kwa kuwa lengo kuu ni kuhakikisha wanamsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassani katika kuwahudumia wananchi na taifa kwa ujumla.    


Naye Waziri Ummy amesema kuwa TAMISEMI sio ngumu bali ni kubwa   lakini ni kubwa kwakuwa     inakupa uwanja mpana  wa kuchagua jinsi gani utakavyoweza   kufanya kazi   kwa kushirikiana na watendaji wengine  ili  kukamilisha malengo yaliyopangwa   kwa wakati huku kila  mmoja akitimiza majukumu yake katika  kutatua changamoto  na kuboresha huduma katika jamii.


Amesema kuwa  uongozi ni kushirikisha wengine ili  waweze kujua muelekeo na maono ya kiongozi wao  lengo likiwa ni kupata matokeo chanya katika utendaji kazi ili  kuboresha  utoaji  huduma kwa  wananchi na kuwataka  watumishi wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI kutoa ushirikiano kwa Waziri Bashungwa ili  kuweza kutimiza majukumu yake  kikamilifu. 


Wakati huohuo Naibu Waziri  Ofisi ya Rais TAMISEMI anayeshughulikia elimu  Mhe. Devid Silinde amemshukuru Waziri Ummy kwa kufanyakazi kwa muda wa miezi tisa lakini ameacha alama isiyofutika kwa jamiia, ambayo ni ujenzi wa madarasa 15,000 ndani ya miezi miwili, kuongeza bajeti ya TARURA KU 273.5  hadi bilioni  966, ujenzi wa vituo vya afya  na Hospitali za Halmashauri.


Vilevile, Naibu Waziri Ofisi ya Rais – TAMISEMI anayeshughulikia afya Mhe Festo Dugange amemshukuru Waziri Ummy kwa kufanyakazi kwa pamoja na kuwa mmoja ya walioleta mabadiliko katika utendaji kazi wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa ndani ya miezi 9 aliyohudumu.

Share To:

Post A Comment: