MBUNGE Catherine Magige 

MBUNGE Lucy Mayenga 

MBUNGE Neema Lugangira 
MBUNGE Munde Tambwe

MBUNGE Esther Malleko

NA MWANDISHI WETU, DODOMA.


Katika Historia ya Tanzania haijawahi kutokea Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano aanzishiwe mchakato wa kutakwa kujiuzulu na Wabunge wake mwenyewe na zaidi ni Wabunge Wanawake Watano (5) Mashujaa ambao jana tarehe 5 Januari 2022 pia walisimama kidete  na kumtikisa Spika Job Ndugai kwa kile walichosema kwamba hawezi tena kuongozo Mhimili wa Bunge maana hakuna tena Mahusiano na Kiongozi wa Mhimili wa Serikali ambae ni Mhe Rais Samia Suluhu Hassan.

Wabunge hao Catherine Magige, Lucy Mayenga, Neema Lugangira, Munde Tambwe na Esther Malleko ambapo kila mmoja kupitia mitandao mbalimbali yakijamii kama instagram, twitter, facebook, na magroup ya whatssup mbalimbali ikiwemo la wabunge ambalo Spika Ndugai mwenyewe alikuwepo  humo  waliandika kuhusu suala la Spika Ndugai wakitaka awajibike na ajiuzulu huku wakisisitiza wanasimama na Mh Rais Samia Suluhu Hassan.

Pia tarehe 6 Januari 2022 tumeshuhudia Matamko ya Wabunge wengi kutaka Spika Ndugai ajiuzulu na hawa ni pamoja na Mariam Ditopile, Lusinde, Askofu Gwajima, Elly Kingu, na Mrisho Gambo. 

Na hivi tunavyoandika leo  tarehe 6 Januari,2022  tayari Spika Ndugai ameandika barua ya kujiuzulu na ikumbukwe hii ni ndani ya Masaa 24 tokea Wabunge Wanawake Watano (5) Mashujaa  Catherine Magige, Lucy Mayenga, Neema Lugangira,Munde Tambwe na Esther Malleko, na Lucy Mayenga kutikisa Bunge na Nchi na kusimama na Mhe Rais Samia Suluhu Hassan. 


- MWISHO -
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: