Mkuu wa wilaya ya Ngorongoro Mhe Raymond Mwangwala amezitaka  taasisi, Mashirika na  Wananchi kupanda miti  kwa wingi hususani  kipindi hiki cha mvua kwani miti inamanufaa makubwa kimqzingira.


Mwangwala amesema hayo wakati akikagua kitalu cha miti zadi ya 600,00 kinachosimamiwa na Wakala huduma  za  Misitu Tanzania ( TFS).

" Ukataji miti hovyo maeneo ya Loliondo haukubaliki ,niwatake Wananchi kufuata utaratibu wa kukata miti tunataka mti mmoja ukikaywa ipandwe miti hata 20"amesema"


Naye Mhifadhi  Misitu Wilaya wa  Ngorongoro (TFS) Bw.Major Ngoilenya amesema TFS imerahisisha upatikanaji wa  Miti  ambapo miti yote inayozalishwa katika  kitalu hicho inatolewa kwa  wananchi bila malipo." Niwakaribishe Wananchi kuja kupata mitii tutunze mazingira yetu" amesema.

Share To:

Post A Comment: