Raisa Said ,Tanga

IMEELEZWA  kuwa  Maambukizi ya Virus vya Ukimwi (VVU) kwa watoto wenye umri wa kuanzia  Miaka 0-5 imepungua kutokana na elimu inayoendelea kutolewa katika Jiji la Tanga.


Kwa Mujibu wa Mratibu wa Ukimwi  Jiji la Tanga Moses Kisibo alisema kuwa elimu katika makundi mbalimbali ikiwemo kwa wajawazito imesaidia kupungiza Maambukizi katika kundi hilo la watoto wadogo.


Kisibo alisema kuwa  kwasasa kundi ambalo ni changamoto ni kundi  la watoto wenye umri wa  Miaka I5 - 35 nakwamba ndilo kundi linaloongoza kwa Maambukizi mapya ambapo kitaifa ni asilimia 40.


Alisema ili kupambana na kundi hilo ni lazima elimu iendelee kutolewa kwa jamii ikiwa ni pamoja na Wazazi kujenga mahusiano ya karibu na watoto wao ili wanapofanyiwa ukatili inakuwa rahisi kuwapatia taarifa.


Katika maadhimio ya  siku ya Ukimwi yaliyofanyika  Dec 1 ,Kimkoa Wilayani Muheza ,Mkuu wa Mkoa  wa Tanga Adam Malima alisema kuwa lengo la Kitaifa na Kidunia ni Ifikapo mwaka 2030 kuhakikisha wanatokomeza Maambukizi mapya ya ugonjwa wa Vvu na Ukimwi.


Katika kuhakikisha lengo hilo linatimia amesema ni lazima kuvunja mtandao  wa ngono zisizo salama  katika makundi  hatarishi jambo ambalo litasaitia pia kuzunguza vifo vitakanavyo na Vvu na ukwimwi.


Malima amewataka  watumishi wote wa Idara ya  Afya walipo katika Halmashauri 11 za Mkoa wa Tanga kuhakikisha wanaendelea na uhamasishaji, utoaji wa elimu kwa jamii juu ya umuhimu wa kupima na kujua afya zao.


Hata hivyo Mkuu wa Mkoa huyo  alitumia fursa hiyo kuitaka jamii kuacha  kunyanyapaa na kubagua  wagonjwa wanaoishi  na ugonjwa huo ambao ni hatari kwa jamii.


Mwisho

Share To:

Post A Comment: