Na. Angela Msimbira TAMISEMI


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali  Mhe Ummy Mwalimu amesema walimu wanaotaka kuhama kutoka mijini kwenda  vijijini ruksa, lakini  wanaohamishwa kutoka  vijijijini kwenda mjini tume  ya  utumishi wa walimu nchini  ihakikishe kabla ya kuwahamisha  wawe na walimu mbadala.


Akifungua mkutano wa baraza la wafanyakazi Tawi la Tume ya Utumishi wa Walimu leo Jijini Dodoma Waziri Ummy amesema kuwa ni marufuku kuhamisha walimu kutoka katika Halmashauri zilizoko pembezoni kabla ya kupeleka waalimu mbadala 


Amesema kuwa uhamisho ni haki ya mtumishi lakini changamoto kubwa wengi wanataka kuhama kutoka Halmashauri za vijijini kwenda mijini, hili haliwezekani, lakini kama amekaa zaidia miaka mitatu na anahitaji kuhama ihakikishwe kunakuwepo na walimu mbadala wa kuziba nafasi inayoachwa na mwalimu anayehama.


Waziri Ummy amesema kuwa Serikali imejikita katika kutoa elimu bora kwa jamii kwa kuhakikisha kunakuwa na mazingira bora ya kufundisha na kujifunzia ni wajibu wa tume sasa kuhakikisha uwiano wa walimu unafanyika ili kutoa elimu sawa kwa watoto wote wa Kitanzania hasa katika Halmashauri zilizopo pembezoni. 


Aidha ameitaka tume ya Utumishi wa Walimu  kufanya tathmini ya kina kwa kuangalia  uwiano wa waalimu kwenye shule  za Msingi na Sekondari katika Mamlaka za Serikali za Mitaa  lengo likiwa ni kuwa na takwimu sahihi za mahitaji halisi ya walimu na uwiano uliosawa katika Halmashauri.

Share To:

Post A Comment: