Na. Angela Msimbira MROGORO


Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe Ummy Mwalimu ameziagiza Halmashauri zote nchini kuiga  mpango wa kuwapanga wamachinga  uliofanywa  na Mkoa wa Morogoro lengo likiwa ni kuwapanga kwa kuwapatia maeneo mazuri ya kufanyia biashara


Ametoa maagizo hayo  leo wakati  akizundua vibanda  vya wafanyabiashara  wadogo  (wamachinga)  uliofanyika katika soko la  chifu Kingalu, Halmashauri ya Manispaa ya Morogoro, Mkoani Morogoro


Waziri Ummy ameupongeza  Mkoa wa Morogoro kwa kuwa  wa kwanza  katika kutekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Mhe. Samia Suluhu Hassani alilolitoa kwenye mkutano wa vijana Jijini Mwanza mnamo tarehe 15/6/2021 hivyo amewaagiza Mikoa mingine kujifunza na kuhakikisha wanatekeleza  maagizo kwa wakati ili kuwapunguzia adha wamachinga ambao wanapata changamoto katika kufanya bishara zao.


Ameendelea kufafanua kuwa dira ya maendeleo ya taifa ya  mwaka imeelekeza kujenga uchumi  unaoakisi  hali halisi ya Mtanzania kwa kukuza viwanda vidogo na vya kati hivyo ili Tanzania ifike na kukua kiuchumi   wafanyabiashara wadogo  lazima kuwa sehemu muhimu ya kukuza uchumi wa nchi


Waziri Ummy wafanyabiasha wadogo  ni muhimu katik kukuza uchumi wan chi, hivyo ni muhimu tukawadhamini na kuwajali  kwa kuwawekea mazingira bora ya kufanyia bishaara kwa kuwatengea maeneo  yaliyobora katika Halmashauri zote nchini


Ameagiza Mikoa yote nchini kuhakikisha wanatenga maeneo kwa ajili ya kuwapanga wamachinga ambao wengi hujishughulisha katika maeneo ambayo si rasmi na hayana usalama katika biashara zao 


Aidha , amesema Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini  ya Rais Samia Suluhu Hassani  itaendelea kudhamini, kuheshimu na kukuza shughuli za wafanyabiashara wadogo wakiwemo wamachinga


Mkoa wa Morogoro unakadiriwa kuwa  na wamachinga  781 ndani ya Mitaa ya mijini waliotambuliwa katika mpango maalum wa kuwapanga wamachinga Mkoani hapo

Share To:

Post A Comment: