NAIBU
 waziri wa maji ,Eng.MaryPrisca Mahundi amemuagiza katibu mkuu wa wizara
 hiyo, atoe fedha za malipo kiasi cha sh .milioni 700 zilizoombwa na 
Wakala wa usambazaji maji safi na usafi wa mazingira vijijini (RUWASA) 
wilaya ya Mkuranga ili kukamilisha ujenzi wa tanki la mradi wa maji 
Mwanambaya.
Ameeleza mradi huu ni miongoni mwa miradi itakayonufaisha watu wengi kwani unakwenda kutoa huduma na kunufaisha watu 8,000 .
MaryPrisca
 alitoa maagizo hayo wakati alipotembelea mradi wa chanzo cha maji 
Mwanambaya na tanki,na kueleza fedha hiyo imeombwa mwezi Juni hivyo 
wavute subira ,katibu mkuu afanyie kazi .
"Niisitize
 miradi inayoelekezwa kutoa huduma kwa wananchi tunaendelea kuitolea 
fedha kwa awamu hadi ikamilike ili kutimiza adhma ya serikali ya kumtua 
ndoo mama kichwani na kuondosha kero sugu ya ukosefu wa upatikanaji wa 
maji
Hata
 hivyo ,ameielekeza RUWASA Mikoa na Wilaya kukamilisha miradi viporo kwa
 wakati ili kurahisisha kazi ya usambazaji kwa wananchi .
Pia
 MaryPrisca ,aliwaelekeza mameneja wa RUWASA mikoa na wilaya kuhakikisha
 jumuiya za watumiaji maji vijijini wanapata watunza hazina makini 
waliosoma uhasibu na kupata cheti ama diploma ili kutunza miradi 
mbalimbali na iwe endelevu .
Nae
 meneja wa RUWASA wilaya ya Mkuranga Maria Malale alisema ujenzi wa 
mradi Mwanambaya umegharimu bilioni 2.3 ambapo bilioni 1.1 amelipwa 
mkandarasi 
Alisema mradi
 umefikia asilimia 90 ,mkandarasi anaendelea na kazi licha ya kupelea 
fedha milioni 700 ambayo wameshaiombea fedha kwa ajili ya malipo.
Mkuu
 wa wilaya ya Mkuranga, Hadija Ally alisema ipo miradi inayoendelea 
ambapo ikikamilika yote hali itakuwa safi na wananchi watanufaika kwa 
kiasi kikubwa na upatikanaji wa maji mjini ni asilimia 86 na vijijini ni
 76.
Katika ziara hiyo ya
 kikazi ,MaryPrisca alitembelea na kukagua pia mradi wa maji Mkerezange 
ambao umekamilika na upo kwenye matazamio .
 
Post A Comment: