
Mbunge wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Neema Lugangira akisisitiza jambo akichangia bajeti ya Wizara ya Kilimo Bungeni Jijini Dodoma
 Mbunge
 wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Neema 
Lugangira akisisitiza jambo akichangia bajeti ya Wizara ya Kilimo Bungeni Jijini Dodoma
Mbunge
 wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Neema 
Lugangira akisisitiza jambo akichangia bajeti ya Wizara ya Kilimo Bungeni Jijini Dodoma NA MWANDISHI WETU, DODOMA
Mbunge
 wa Viti Maalumu kupitia Asasi za Kiraia Tanzania Bara (NGOs) Neema 
Lugangira ameitaka Wizara ya Kilimo iache kuimba wimbo wa Bei ya Mkulima
 badala yake watoke huko waende kwenye Pato la Mkulima ili kuongeza tija
 kubwa kwenye sekta hiyo.
Aliyasema
 hayo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akichangia Bajeti ya Wizara ya 
Kilimo ambapo Mbunge Neema alisema kwa kipindi kirefu Wizarani wamekuwa 
wakiongelea tu Bei ya Mkulima lakini wakati umefika sasa waongelee Pato 
la Mkulima kwa sababu wanapoongelea Pato la Mkulima lina faida mbili ya 
kwanza ni bei na ya pili ni wingi na ubora yaani kimahesabu Pato la 
Mkulima lina Variables mbili = Price/Bei x (Quantity/Wingi + 
Quality/Ubora). 
Alisema 
kwamba Wizara ya Kilimo wamekuwa wakiweka jitihada kwenye Bei ya Mkulima
 na sasa ameishauri Wizara ikumbuke hii Variable ya ya pili ya Q ambayo 
ni Quanity/Wingi na Quality/Ubora.
Mbunge
 Neema aliendelea kwa kusema kwamba kwa sababu Wabunge wengi wameongelea
 tija yetu ya kwenye kilimo anapenda kutoa mifano miwili: Kwa wenzetu wa
 Zambia wanauza kilo moja ya mahindi wanauza TZS. 250 mpaka 300 na 
wakiuza kwa bei hiyo wanarudisha gharama zao yaani wamefikia break-even 
point lakini kwetu sisi Tanzania ili kufikia kiwango cha break-even 
lazima tuuze kilo moja ya mahindi TZS.500 .
“Hivyo
 hivyo hata kwenye Pamba kwa nchi ambazo tunashindana nazo India, 
Brazili, China , Egypt wao wanazalisha eka moja kilo 1,000 hadi 1,250 na
 wao wakiingia sokoni wanaweza kuuza kwa bei ya TZS..500 kwa kilo na kwa
 kiwango hiko wamekuwa wamefikia kiwango cha break-even lakini sisi kwa 
sababu tija yetu ni ndogo tunazalisha eka hiyo hiyo moja kilo 250 hivyo 
hatuwezi kuuza kwa bei ya TZS 500 yaani mpaka ifike angalau TZS 1000” 
Alisema
Mbunge huyo 
alipendekeza kwamba ifika wakati Wizara ya Kilimo ianze kuongelea Pato 
la Mkulima na sio Bei ya Mkulima kwani kufanya hivyo wataweza kuongeza 
tija ambayo itaongeza mchango wa Sekta ya Kilimo kwenye Pato la Taifa 
kwa sababu wamekuwa wakisema asilimia 65 ya watanzania wapo kwenye 
Kilimo lakini bado Sekta ya Kilimo inachangia asilimia 27 tu kwenye Pato
 la Taifa. 
Mbunge 
Lugangira alisisitiza kwamba kama Wizara itaendelea na Wimbo wa Bei ya 
Mkulima basi itakuwa inaendelea kufidia upungufu wetu wa tija kupitia 
Bei ya Mkulima jambo ambalo sio sahihi kwahiyo ni lazima sasa Wizara ya 
Kilimo ijikite katika Pato la Mkulima.
Hata
 hivyo pia Mbunge Lugangira aliishauri Wizara ya Kilimo ipitie upya 
Vituo vya Rasilimali ya Kilimo Ngazi ya Kata “Ward Agriculture Resource 
Centres” ione kama Vituo vinatumika kadiri ambavyo ilitakiwa na kama 
kuna  changamoto virudishwe kuwa chini ya Wizara ya Kilimo ili viweze 
kuchangia katika kukuza tija kubwa ya kilimo kama ilivyokusudiwa.
Kutokana
 na kwamba Vituo hivyo vilikuwepo kwa miaka mingi na Halmashauri 
zimekuwa hazitengi Bajeti ya Huduma ya Ugani jambo ambalo ni changamoto 
kubwa katika uendelezaji wa kada hiyo muhimu kwa maendeleo ya kilimo 
nchini.
“Kwanza 
nakushukuru sana Mh Spika kwa kunipa nafasi ya kuchangia kwenye Bajeti 
ya Wizara ya Kilimo na naomba nianza kwa kusema naunga mkono Hoja. Sera 
ya Kilimo hapa nchini inasema Mgani mmoja Kijiji kimoja kama 
tunavyofahamu kuna Vijiji takribani elfu 12000 na tuna Wagani elfu 7000 
kwa sasa nchini hivyo tuna upungfu Wagani elfu  5000” Alisema
“Lakini
 pia napenda kuipongeza Serikali kupitia Wizara ya Kilimo hususani 
Waziri Profesa Adolf Mkenda na Naibu Waziri wake Hussein Bashe kwa 
jitihada kubwa walizoweka kuleta Mageuzi kwenye Huduma za Ugani ikiwemo 
kutenga Bajeti kwa ajili ya kuwanulilia Maafisa Ugani vitendea kazi kama
 pikipiki, nawapongeza sana lakini bado kuna changamoto ambayo mimi 
ninaiona na kwamba bado Wizara ya Kilimo inategemea Afisa Ugani huyo awe
 mtaalamu kwa kila kitu ajue mazao yote, mbolea, wadudu,masuala ya 
madawa, fangazi, ukungu na nk jambo ambalo sio rahisi” Alisema
Mbunge
 Neema Lugangira alisema Serikali iliamua kuanzisha Vituo vya Rasilimali
 ya Kilimo Ngazi ya Kata ili viweze kuwa na tija kubwa kwenye kilimo na 
kama sikosei vituo hivyo vilianzishwa kwenye Kata 200 hapa nchini na 
pamoja na kuanzishwa Serikali iliweka wataalamu kwenye vituo hivyo, 
vitendea kazi kama kompyuta, Jenereta, screen za kufundishia nk,
“Katika
 hili niwapongeze Wizara ya Kilimo maana nimeskia kupitia Hotuba ya 
Waziri wa Kilimo Profesa Adolf Mkenda kwamba wanakwenda kufufua Vituo 
hivyo lakini ningependa kushauri lazima Wizara ihakikishe Vituo hivyo 
viweze kufanya kazi ambayo imekusudiwa kwa sababu hivi sasa Vituo hivyo 
vipo chini ya Halmashauri kwenye Halmashauri nyingi vituo hivyo 
havifanyi kazi iliyokusudiwa ya kuendeleza kilimo kwa mfano Kituo 
kilichopo Chamwino badala ya kufanya kazi ya kuendeleza kilimo inatumika
 na TARURA" Alisema.
Alisema
 pia hawawezi kuendeleza Kilimo wakati hizo Halmashauri ambazo karibia 
asilimia 70 ya Mapato yake ya Ndani yanatokana na Kilimo lakini Utengaji
 wa Bajeti ya Huduma ya Ugani hawatengi na kwakuwa suala hili linahusu 
Ofisi ya Rais TAMISEMI na Waziri yupo Bungeni anaskia  pengine 
atawaambia wanapanga vipi kuhakikisha hizo Halmashauri zinatenga Bajeti 
ya Huduma ya Ugani.
“Na 
mimi naamini lengo zima la kuanzishwa Vituo hivyo ilikuwa ni kuhakikisha
 wanaimarisha Huduma ya Ugani na wakifanya hivyo wataweza kuongeza tija 
na muhimu zaidi kuongeza Pato la Mkulima.
Mbunge
 Lugangira alimaliza kwa kusisitiza: "Kwa muda mrefu tumekuwa 
tukiongelea Bei la Mkulima na kabla sijaingia hapa Bungeni nilikuwa 
nafanya kazi kwenye Shirika ambalo lipo chini ya Wizara ya kilimo la 
SAGCOT (Southern Agricultural Growth Corridor of Tanzania) kama 
Mkurugenzi wa Idara ya Sera na nimefurahi nimemuona bosi wangu Mr. 
Geoffrey Kirenga yupo kwenye Ukumbi wa Bunge kwa hiyo naendelea 
kusisitiza Wizara ya Kilimo iache Wimbo wa Bei ya Mkulima na ijikite 
katika Pato la Mkulima” Alisema

Post A Comment: