![]()  | 
| WAZIRI 
Mkuu Kassim Majaliwa akisisitiza jambo leo Bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu maswali papo kwa hapo ya wabunge | 
WAZIRI 
Mkuu Kassim Majaliwa amesema Serikali imekuwa ikitumia Balozi zake za 
nje kutangaza mazao yaliypo ndani ya nchini ili kuweza kuyauza kwenye 
nchi ambazo wanatumia mazao hayo hatua ambayo imepelekea kupata wateja 
wengi kuja kununua hali iliyosaidia kuimarika kwa masoko.
Aliyasema
 hayo Bungeni Mjini Dodoma wakati akijibu swali la papo kwa hapo la 
Mbunge wa Viti Maalumu ( CCM) kupitia NGOs Mh Neema Lugangira ambapo 
aliuliza kutokana na uwepo tatizo kubwa la masoko ya mazao yaliyopo 
nchini hata kama wakulima wanazalisha kwa ubora wa hali ya juu.
Je
 Serikali ipo tayari kupelekea wataalamu wake kwenye nchi ambazo 
zimefanikiwa ili kujifunza namna bora ya usimamizi wa masoko yaliyopo
Waziri
 Mkuu Majaliwa alisema kwamba muhimu ni kutafuta mfumo mzuri unaowezesha
 mazao yaliyopo kujulikana na kuyauza kwenye nchi ambazo kuna wateja na 
wapate bei nzuri kama ilivyo ndani ya nchi uwepo mfumo wa stakabahdi 
ghalani ambao unakusanya mazao pamoja na kuwaalika wanunuzi wanakuja 
kila mmoja anatamka atanunua zao hilo kwa bei gani hivyo yule mwenye bei
 ya juu anapata fursa kununua. 
Alisema
 kwamba huo ni ni mfumo uliondaliwa kwa ajili ya uuzaji wa mazao na 
utakuwa na bei nzuri huku akieleza pia Serikali ina mpango wa kutafuta 
masoko kwenye nchi ambazo zinazohitaji mazao hayo ili kuhakikisha 
wakulima wananufaika na kuweza kujikwamua kiuchumi
 “Juzi
 nilikuwa na Wabunge wa Mkoa wa Rukwa wakiomba Serikali iwasaidie kufika
 nchi ya Kongo, Zambia, Rwanda na Burundi kutafuta masoko ya mazao 
yanayolimwa mkoani humo” Alisema Waziri Mkuu
Aidha
 alisema kazi inayofanywa kwa sasa na Serikali ni kuhakisha inawasiliana
 na nchi ambazo ni walaji wa mazao hayo ili kujihakikisha mazao hayo 
yanapolimwa na kuvunwa yanapelekwa kwenye nchi zao na hiyo ni njia ya 
kupata soko nzuri la mazao pamoja na ubora unaofanywa. 
Alisema
 kwa sasa Serikali itaendelea kujenga masoko ya kimkakati na ya kikanda 
ambayo yanalengwa pembezoni mwa nchi ili kukaribisha waliopo jirani 
kwenda kununua mazao yanayozalishwa hapa nchini
“Lakini
 miezi mitatu iliyopita nilikuwa Kilimanjaro pale Holili wanajenga soko 
kubwa sana ambalo wananchi wanaozalisha mazao yanapelekwa hapo na watu 
wa nchi jirani watakwenda hapo kununua  na wanawapunguzia ugumu wa 
kuingia mpaka ndani”Alisema
Hata
 hivyo alisema mwezi mmoja uliopita alikuwa mkoani Kigoma ambapo eneo 
Kagunda wamejenga soko nzuri wanawakaribisha majirani watu wa Burundi na
 Rwanda kwenye kununua jambo ambalo linapunguza umbali wa kufuata 
bidhaa.
Sambamba
 na hilo alieleza kwamba hivi sasa Serikali inajenga soko kubwa mkoani 
Kagera eneo la Nyakanazi lengo wale wanaotoa Kongo, Rwanda watafika 
kwenye soko hilo la zaidi ya Bilioni 3.5 ili waweze kupata bidhaa na 
muhimu ni kuweka mkakati wa namna mazao yaliyoboreshwa na kupata thamani
 kubwa ili yaweza kupata thamani kubwa ili kumuwezesha mkulima aweze 
kupata tija kwa kazi ya kilimo anayoifanya.
Mwisho



Post A Comment: