Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), limetoa sababu ya kubadilisha Mwamuzi atakayechezesha mchezo wa Simba SC na TP Mazembe ya Congo.

Taarifa imesema kuwa baada ya Primero ya Angola kuitoa TP Mazembe katika robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika msimu uliopita, wakakutana na Esperance ya Tunisia na Mwamuzi Jani Sikazwe wa Zambia ndiye akaamua mechi ya pili iliyowang'oa Waangola hao ambao walilalamika CAF na Sikazwe akasimamishwa.

Sasa CAF wameipa Simba Sikazwe na kumuondoa mwamuzi kutoka Ethiopia.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: