CHUO
 cha Uhasibu Arusha(AII)kinatarajia kuanzisha programu mpya nne za 
Uzamili kwa fani ambazo zitawawezesha wahitimu kukubalika kwa urahisi 
katika soko la ajira za moja kwa moja nchini.
Hayo
 yamesemwa leo na Kaimu Mkurugenzi wa Chuo Uhasibu Arusha Dk. Samwel 
Welema wakati anazungumza na wadau kutoka katika mashirika na kampuni 
mbalimbali za binafsi na Serikali katika warsha iliyofanyika kwenye Chuo
 hicho Kitivo cha Dar es Salaam.
Amefafanua
 kuanzishwa kwa program  hizo kitakiwezesha chuo hicho kujihakikishia 
kwamba kile kinachofundishwa kitaenda kutumika na kinauhitaji mkubwa 
kwenye soko la ajira.
Dk.Welema
 amezitaja programu hizo ni Master of Science and 
Investment(MScFI),Master in Business Administration(MBA), Master in 
Business Administration in Information Technology Management(MBA-ITM) na
 Master of Business Administration in Procurement and Supplies 
Management(MBA- PSM)
Kwa
 upande wa Mkuu wa Idara ya Masomo ya Uzamili chuoni hapo, Grace Temba 
amesema, michango na maoni mbalimbali waliyoipata kutoka kwa wadau 
wakitaka kuanzishwa kwa program hizo mpya na ndio sababu ya chuo hicho 
kuona haja ya kuanzisha program hizo.
"Kwa
 kipindi cha miaka mitatu...minne, tumeweza kuongeza kusomesha walimu 
wetu hadi kufikia 16 ambao wanadigrii na wapo tayari kutoa elimu kwa 
hatua ya Uzamili" amesema Temba.
Amesema,
 wamepata maoni kutoka kwa wawakilishi wa mashirika na kampuni mbali 
mbali na lengo kuu ni kuhakikisha  kile ambacho kinaenda kutumika 
kinamahitaji kwenye soko la ajira.
Ameongeza,
 wahitimu wengi wanamaliza wakiwa wanajua nadharia tu, lakini sasa chuo 
kitakuwa kinatoa mafunzo kwa vitendo ambapo wahitimu watakuwa na uwezo 
mkubwa ukiwemo kuandaa ripoti, kusaidia kampuni na kuchanganua masuala 
mbalimbali kwa manufaa ya kampuni.
 Kaimu
 Mkuu wa chuo cha Uhasibu cha Arusha, (AII),  Dk. Samwel Welema 
akizungumza na wadau kutoka mashirika na makampuni mbali mbali nchini, 
juu ya azma ya chuo hicho kuanzisha programu nne za uzamili, katika 
warsha iliyofanyika katika chuo hicho kitivo cha Dar es Salaam.
 Mhadhiri
 wa chuo cha Uhasibu Arusha Kitivo cha Dar es Salaam, Allan Msola 
akiwaelezea wadau kutoka mashirika na makampuni mbali mbali nchini juu 
ya  programu nne za uzamili zinazotarajiwa kuanzishwa na chuo hicho hivi
 karibuni hapa nchini, katika warsha iliyofanyika katika chuo hicho 
kitivo cha Dar es Salaam.
Wadau na washiriki kutoka kwenye makampuni na mashirika mbali mbali wakifuatilia kwa making warsha iliyotolewa na chuo cha Uhasibu Arusha (AII) juu ya namna program mpya za uzamili zinazotarajiwa kuanzishwa na chuo hicho zitakavyowanufaisha wahitimu na makampuni watakayoenda kufanyia kazi.
Wadau na washiriki kutoka kwenye makampuni na mashirika mbali mbali wakifuatilia kwa making warsha iliyotolewa na chuo cha Uhasibu Arusha (AII) juu ya namna program mpya za uzamili zinazotarajiwa kuanzishwa na chuo hicho zitakavyowanufaisha wahitimu na makampuni watakayoenda kufanyia kazi.
Mkuu
 wa Idara ya masomo ya Uzamili wa chuo cha Uhasibu Arusha(AII), Grace 
Temba,akifafanua juu namna Program mpya zinazotarajiwa kuanzishwa na 
chuo hicho zitakavyofanya kazi na kuwawezesha wahitimu kukubalika moja 
kwa moja kwenye soko la ajira ndani na nje ya nchi





Post A Comment: