Home
SIASA
MWENYEKITI WA BUNGE AMWOMBA RADHI MBOWE
Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Zungu amemuomba radhi kiongozi wa
Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe kwa kushindwa kutambua
mchango wake kwa waathirika wa tetemeko la ardhi mkoani Kagera.
Hatua
hiyo imefutia mwongozo ulioombwa na wabunge wawili Chadema, kuwa
mchango wa Mbowe haukutambulika licha ya kufika Bukoba, kutoa misaada na
kushirikiana na waathirika wa tukio hilo hadi sasa.
Aliyeanza
kuomba mwongozo ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ambaye alihoji
kwa nini mwenyekiti huyo wa Bunge amewatambua viongozi waliofika eneo la
tukio na kutoa misaada lakini ameshindwa kumtambua Mbowe ambaye mpaka
sasa yupo eneo la tukio na ametoa msaada.
Mbunge mwingine ni
Pascal Haonga wa Mbozi ambaye alisema Mbowe ni kiongozi mkubwa na
halitakuwa jambo la maana kama mchango wake hautatambulika kwani suala
hilo siyo la kisiasa.
Kufuatia mwongozo huo, Zungu aliomba radhi na kuongeza kuwa anamtambua Mbowe kama kiongozi aliyetoa msaada kwa waathirika hao.
Awali,
Mwenyekiti huyo wa Bunge baada ya kuingia ukumbini alitoa pole kwa
waathirika wa tetemeko hilo lililoua watu 17 na kuwatambua watu
waliochangia tukio hilo akiwamo Waziri Mkuu Kassim Majaliwa na
wafanyabiashara. Baada ya kipindi cha maswali na majibu kuisha,
mwenyekiti huyo aliwatambua wafanyabiashara wengine waliotoa msaada kwa
waathirika hao lakini hakugusia msaada ulitolewa na Mbowe.
www.msumbanews.blogspot.com
Back To Top
Post A Comment: