Home
SIASA
Maswali yaibuka kuhusu ni vipi Zuma alipata mkopo wa kulipa deni 
 
            
            
        
Maswali yameibuka nchini Afrika Kusini kuhusu mkopo 
aliopewa rais wa nchi hiyo Jacob Zuma, na benki isiyo maarufu ya VBS 
kulipa deni lililotokana na ukarabati uliofanyiwa nyumba yake binafsi 
huko Nkandla.
Ofisi ya rais ilitoa taarifa siku ya Jumatatu, 
ikitangaza kuwa bwana Zuma alikuwa ametuma fedha hizo ambazo ni zaid ya 
dola 500,000 kweneda  benki ya SARB. Hii ni kufuatia amri iliyotolewa na
 mahakama ya katiba mwishoni mwa mwezi Machi.
Bwana Zuma atalipa mkopo huo ndani ya kipindi cha miaka 20 inayokuja.
 
Kulingana na magazeti ya nchi hiyo, baadhi yanauliza ni vipi Zuma 
mwenye umri wa miaka 74 aliweza kupata mkopo huo ulio zaidi ya mapato 
yake na ikiwa ni kisa cha kutoa mkopo kwa njia ya kiholela.
Benki hiyo inayomilikiwa na watu weusi inaripotiwa kuwa na matawi manne tu kote nchini humo.
Wakati uo huo chama cha upinznania cha Democratic Alliance kimetaka kuona ahakaiksha kuwa deni hilo limelipwa.
 
 
 
 
  
 
 
 
 
 
 
 
 
 Back To Top
 
Post A Comment: