Mbunge wa viti maalum mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) DR Ritta Kabati akiongea na wanawake wa mkoa wa Iringa wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.Mbunge wa viti maalum mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) DR Ritta Kabati akiwa na mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake.
 Baadhi ya wanawake wa mkoa wa Iringa wakiwa kwenye maandano ya kusherekea siku ya wanawake duniani.


Na Fredy Mgunda,Iringa.

 

MBUNGE wa viti maalum mkoani Iringa kupitia chama cha mapinduzi (CCM) DR Ritta Kabati alisema licha ya wanawake kudai masuala ya Usawa wa kijinsia ni muhimu wakatambua kuwa usawa unaozungumzwa ni nafasi katika vyombo vya maamuzi na si katika ngazi ya familia kulingana na mila na desturi Zilizopo

Akizungumzia maadhimisho ya siku ya mwananmke Duniani Dr kabati alisema baadhi ya wananwake wamekosa uelewa wa kutosha kuhusu mkakati wa kufikia lengo la usawa wa kijinsia hali inayochochea wanawake walio wengi kuwa chanzo chas kuvunjika kwa ndoa

Dr Kabati alisema kuwa wanawake wanatakiwa kuendelea kutekeleza wajibu wao kama wanawake katika familia ikiwepo kuwaheshimu na kuwashirikisha kwenye majukumu mbalimbali waume zao ili kudumisha ndoa zao kwa kuwa wanaume ni kichwa cha familia.

Aliwataka wanawake kuacha tabia ya ulimbukeni kutokana na kipato na nyazifa walizonazo katika jamii badala yake wanatakiwa kuendelea kutimiza wajibu kwa wanaume zao kama ambavyo mila na desturi zinavyosema.

Dr kabati alisema kuwa wanawake wengi hawajitambui ndio maana ndoa nyingi kwa miaka ya hivi sasa zimekuwa zikivunjika bila sasababu za msingi kutokana na wanawake kuto waheshimu wanaume zao.

Alisema kuwa analaani tabia ya wanawake ambao wamekuwa wanafanyia tabia za dharau wanaume zao ambao ndio kichwa cha familia na ndio kimekuwa chanzo kikubwa cha migogoro ya familia hivi sasa duniani.

Dr Kabati alisema kuwa wanawake wanatakiwa kuwatunzia siri wanaume zao hata kama wamewazidi madaraka na kipato hapo ndio ndoa itadumu kwa amani kwa sababu mke unakuwa umeshuka kwa mume wako.

Alisema kuwa jambo la hamsini kwa hamsini kwa ngazi ya familia haliwezekani kutokana na mira na destori za kiafrika kwa kuwa wanawake kutolewa mahari na wanaolewa  hali ambayo inaweka wazi kuwa mwanaume ndio kiongozi mkuu wa familia hata kama kipato chake ni kidogo.

 

Dr Kabati alisema wanawake wengi waliofanikiwa kwenye nafasi mbalimbali ni wale waliojishusha na kuwashirikisha wanaume zao hata kama wanavipato vidogo,kuheshimia na kuthaminia hapo itasaidia kuleta amnai kwenye ndoa.

 

Alimalizia kwa kusema kuwa wanawake wanatakiwa kuhakikisha wanawalea watoto wao kwenye malezi yanayotakiwa katika jamii ili kuwa na kizazi ambacho kitakuwa na maadili katika jamiii.

 

 

 

 

 

 

 

Share To:

Post A Comment: