Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imempongeza Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema, Mkuu wa Wilaya ya Kahama Festo Kiswaga na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kahama Anderson Msumba kwa kazi nzuri ya kutekeleza miradi yake katika Halmashauri hiyo.

Makamu Mwenyekiti Mhe. Selemani Zedi aliyasema hayo wakati akihitimisha ziara ya kamati ya siku mbili Halmashauri ya Manispaa ya Kahama.

Mwenyekiti alisema amefurahi kuona asilimia kumi iliyotengwa kwenye fedha za Halmashauri zinaenda kwa akina mama na walemavu kama ilivyokusudiwa.

Kamati ilishauri wanufaika wa saccos za kina mama waongezeke na pia Mkurugenzi aangalie utaratibu wa kuwapa mikopo vijana ili waweze kujiendeleza kibiashara.

Pia Kamati iliridhishwa na kasi ya mradi wa Hospitali ya OPD- Hospitali ya Manispaa ya Kahama ambayo ujenzi wake umekamilika kwa zaidi ya asilimia 95 na kuahidi kukabidhi ndani ya siku 13.

Kwa upande wa vijana wa Sacco wamemshukuru sana Mhe. Rais Mama Samia kwa mikopo hii wanayoletewa kwa wakati na Mkurugenzi kuahidi kuwaongezea fedha za mikopo hiyo.

Share To:

Post A Comment: