Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaji Majid Hemed Mwanga (Katikati) akizungumza kwenye ziara hiyo katika Kijiji cha Kitunduweta .Kulia kwake ni Mkurugenzi Mtedaji wa wilaya Kisena Mabula kushoto kwake ni Mwenyekiti Wa Halmashauri hiyo Mhe. Wilfred Sumari.

Meneja wa Mradi wa Mkaa endelevu, Charles Lyimo akieleza malengo ya Mradi huo mbele ya viongozi wa wilaya na madiwani.

Katibu wa kamati ya maaliasili ya Kijiji cha Kitunduweta, Leoti Msoloka aliyevaa nguo za kijani akieleza mafanikio ya mradi na namna wanavyofanya shughuli za uvunaji.
Katibu wa wachoma Mkaa katika Kijiji cha Kiotunduweta,Kulangwa Ganga akieleza namna wanavyopata eneo na wanavyochoma Mkaa kupitia matanuri hayo ya kisasa waliyofundishwa ya kuchomea mkaa.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Alhaji Majid Hemed Mwanga akiwa amesimama juu ya Tanuri la mkaa ambalo linaendelea kupangwa.
Madiwani pamoja na viongozi wengine walioshiriki ziara hiyo wakifuatilia maelezo ya utekelezaji wa mradi pamoja na kuuliza maswali ili kupata ufafanuzi Zaidi kuhusu namna wanavyonufaika na mfumo huo.
Madiwani pamoja na viongozi wengine walioshiriki ziara hiyo wakifuatilia maelezo ya utekelezaji wa mradi pamoja na kuuliza maswali ili kupata ufafanuzi Zaidi kuhusu namna wanavyonufaika na mfumo huo.
Ziara ikiendelea.
Madiwani pamoja na viongozi wengine walioshiriki ziara hiyo wakifuatilia maelezo ya utekelezaji wa mradi pamoja na kuuliza maswali ili kupata ufafanuzi Zaidi kuhusu namna wanavyonufaika na mfumo huo.
 

Na Calvin Gwabara, Kilosa


MKUU wa Wilaya ya Kilosa Mkoani Morogoro Alhaji Majid Hemed Mwanga amesema wilaya yake haitamvumilia wala kumfumbia macho kiongozi au Mwananchi yeyote atakayecheza na rasilimali za Misitu kwa kufanya kinyume na utaratibu uliowekwa kwenye vijiji vilivyo chini ya mpango wa usimamizi shirikishi wa Misitu ya Vijiji na vile ambavyo bado havijaingia kwenye mpango huo.

Wito huo ameutoa wakati wa ziara aliyoifanya na kamati ya Ulinzi Usalama,Madiwani na viongozi wa Mashirika ya TFCG na MJUMITA katika Kijiji cha Kitunduweta wilayani humo  ili kujionea namna mashirika hayo yanavyotekeleza mapango wa isimamizi shirikishi wa misitu kwenye vijiji 20 vya Wilaya hiyo na kusikia shuhuda na mafanikio na kazi kubwa zilizofanywa na mashirika hayo katika kufikia mafanikio hayo.

”Kwakweli kazi kubwa sana imefanywa na wadau wetu Shirika la kuhifadhi Misitu ya asili Tanzania (TFCG) na Mtandao wa Jamii usimamizi wa misitu Tanzania (MJUMITA) na sasa kazi iliyobaki ni sisi kuhakikisha elimu tuliyoipata inaednelea kuleta matokeo chanya katika kutunza misitu yetu, na niseme tu kwamba fedha nyingi mnapata kwenye vijiji lakini naomba mtambue kuwa fedha hizo ni fedha za Umma zitumike kwa kufuata taratibu zote za matumizi ya fedha za Umma na Ssio vinginevyo maana ninaz taarifa kuwa baadhi ya viongozi wanatumia fedha hizo vibaya na kuna vijiji kamati zake kama Kijiji cha Ihombwe imeivunja” Alisisitiza Alhaj Mwanga.

Mkuu huyo wa Wilaya aliwataka Wananchi kwenye vijiji hivyo kutowafumbia macho viongozi wanaovuruga utaratibu mzuri ulioanzishwa bali watoe taarifa kwenye ofisi yake na mamlaka zingine ili washughulikiwe na kuwasisitiza kuendelea kuhifadhi misitu hiyo ya vijiji na kuitumia kwa uendelevu na kwa maslahi mapata ya vijiji na Taifa.

“Nyinyi sasa ni Walimu maana tumeona wenzenu kutoka kwenye Wilaya ya Ruangwa anakotoka Waziri Mkuu wetu walikuja kujifunza kutoka kwenye Kijiji chenu sasa tuache kulalamika na kunedelea kulilia mafunzo Zaidi maana tunataka sasa hawa wadau wahamie kwenye vijiji vingine kwenye wilaya yet una mikoa mingine ili elimu hii ifike nchi nzima, tunachotaka sasa ni kuona nyinyi mnasonga mbele kama walimu” Aliongeza Mkuu huyo wa wilaya ya Kilosa.

 Alhaj Mwanga amewataka kuacha kusikiliza maneno ya baadhi ya watu wanaokuja kuharibu misitu na kuharibu taratibu zilizowekwa wakisingizia kuwa ni maagizo kutoka kwa wakubwa na kuwataka waache kuwasiliza maana hauna maagizo yoyote yanayotoka juu kwenye kuharibu misitu na akitokea mtu huyo watoe taarifa haraka ili watu hao wakamatwe na kuchukuliwa hatua.

Mkuu huyo wa Wilaya ya Kilosa amewasisitiza viongozi wa Kijiji na kamati za maliasili kila mmoja kutambua majukumu yake na kuacha kuingilia kwenye majukumu ili kuondaa migogoro isiyo ya lazima ambayo inatokana na hela wanazozipata kutokana na mapatoa yanayokusanywa kwenye tozo na fedha za misitu.

Akieleza malengo ya Mradi huo Meneja wa Mradi wa Mkaa endelevu Charles Lyimo amesema lengo kuu ni kuhifadhi Misitu ya vijiji kikamilifu kutokana na tafiti kuonesha kuwa kwa mwaka Tanzania tunapoteza hekta 460,000 za misitu kutokana na shughuli mbalimbali za uchomaji Mkaa, Kuni,Kilimo na Mbao na kiasi kikubwa cha upotevu huo kinafanyika kwenye ardhi za vijiji katika maeneo ambayo hayajahifadhiwa.

Ameongeza kuwa katika kufanikisha hilo Mradi unawezesha vijiji pamoja na Wilaya kuweza kuziwekea mpango bora wa kusimamia rasilimali hizo za mistu vizuri ili kunufaika nazo kama vijiji lakini pia Serikali kwa ujumla.

Meneja huyo wa Mradi amesema lengo la pili ni kuchangia kwenye maendeleo ya Wananchi maana hiyo ndiyo sera ya Serikali kwamba wananchi wanaoishi pembeni mwa rasilimali za mistu waweze kunufaika nazo kwa njia endelevu nah ii ni katika kuwaonesha Wananchi kuona rasilimali hiyo ya misitu ni yao na wana jukumu la kuilinda na kuihifadh kwakuwa wanapata motisha.

”Kupitia program hii ya uhifadhi shrikishi wa misitu tunaona kwamba kuna haja ya kuzidi kuiendeleza na jukumu kubwa tulilonalo hasa katika awamu hii ya tatu ya mradi huu tayari tumeshaanza kuondoka kwenye vijiji vya awali na wilaya ya Kilosa sasa tunahamia kwenye wilaya zingine nje ya mkoa wa Morogoro na tumewaachia halmashauri ya Wilaya ili waweze kuwasimamia na kuratibu hivi vijiji”Alibainisha meneja wa Mradi.

Katibu wa kamati ya maaliasili ya Kijiji cha Kitunduweta, Leoti Msoloka amesema kupitia Usimaizi shirikishi wa Misitu ya Kijiji chao wamepata mafanikio makubwa ikiwemo ujenzi wa Ofisi ya Kijiji, Ukatabati wa vyumba vya madarasa,Ujenzi wa matundu ya vyoo pamoja na kuwakatia bima ya afya iliyoboreshwa Wanakijiji wote kijijini hapo ambapo sasa wamenza na ujenzi wa Zahanati ya Kijiji ili wapate huduma kijijini kwao.

“Faida kubwa ni kwamba hapo awali tulikuwa hatujui umuhimu wa kuhifadhi Msitu wa Kijiji lakini baada ya elimu na faida tulizozipata na sasa asilimia tisini ya mapato yatokanayo na misitu zinatumika kijijini tofauti nah apo awali ambapo asilimia hizo zilikuwa zinaenda wilayani na sasa tunaweza kuzitumia fedha hizo kulinda msitu na kunufaisha Kijiji chetu” Alifafanua bwana Msoloka.

Mradi huu wa uhifadhi shirikishi wa misitu ya vijiji unatekelezwa na shirika la kuhifadhi Misitu ya asili Tanzania (TFCG) na Mtandao wa Jamii usimamizi wa misitu Tanzania (MJUMITA) kwa ufadhili wa shirika la Maendeleo la USWISI (SDC).

 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: