.
Mkuu
wa wilaya ya Malinyi Mathayo Masele akizungumza jambo kwenye Kikao cha
kutoa mrejesho wa Utafiti wa Madini uliofanyika katika eneo la Lumbanga
wilayani Malinyi mkoa wa Morogoro.
Kaimu
Mkurugenzi wa Jiolojia wa GST Maswi Solomon Mwita akizungumza jambo
kwenye Kikao cha kutoa mrejesho wa Utafiti wa Madini uliofanyika katika
eneo la Lumbanga wilayani Malinyi mkoa wa Morogoro.
Mjiolojia Mwandamizi wa GST Zortasy Mpangile Maganga akiwasilisha taarifa ya utafiti uliofanyika katika eneo la Lumbanga wilayani Malinyi mkoa wa Morogoro
Mjiolojia
Mwandamizi wa GST Zortasy Mpangile Maganga akiwasilisha taarifa ya
utafiti uliofanyika katika eneo la Lumbanga wilayani Malinyi mkoa wa
Morogoro.
Mjiolojia
wa GST Onesphorius Balambirwa akizungumza jambo kwenye Kikao cha kutoa
mrejesho wa Utafiti wa Madini uliofanyika katika eneo la Lumbanga
wilayani Malinyi mkoa wa Morogoro.
Baadhi
ya wataalamu wa GST wakijadili jambo na Mkuu wa Wilaya ya Malinyi
Mathayo Masele mara baada ya Kikao cha kutoa mrejesho wa Utafiti wa
Madini uliofanyika katika eneo la Lumbanga wilayani Malinyi.
Mjiolojia
Mwandamizi wa GST Zortasy Mpangile Maganga akiwasilisha taarifa ya
utafiti uliofanyika katika eneo la Lumbanga wilayani Malinyi mkoa wa
Morogoro.
Kaimu
Mkurugenzi wa Jiolojia wa GST Maswi Solomon Mwita akizungumza jambo
kwenye Kikao cha kutoa mrejesho wa Utafiti wa Madini uliofanyika katika
eneo la Lumbanga wilayani Malinyi mkoa wa Morogoro.
Baadhi
ya wajumbe walioshiriki kikao cha kutoa mrejesho wa Utafiti wa Madini
uliofanyika katika eneo la Lumbanga wilayani Malinyi mkoa wa Morogoro
wakiwa kwenye picha ya pamoja katika jingo la offisi ya Mkuu wa wilaya
ya Malinyi Mathayo Masele.
Na Tito Mselem-WM
Mkuu
wa Wilaya ya Malinyi,Mathayo Masele ametoa wito kwa Taasisi ya Jiolojia
na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) kuendelea kuitangaza Wilaya ya
Malinyi baada ya kugundulika kuwa na uwepo wa madini ya dhahabu ili
kuwavutia wawekezaji wilayani humo.
Akizungumza
katika kikao cha kupokea mrejesho wa utafiti uliofanywa na GST wilayani
Malinyi, Masele amesema kuwa, wilaya yake sasa imeingia kwenye ramani
ya kuwa na madini ya dhahabu hivyo amewataka wananchi wa wilaya hiyo
kuitumia fursa ya uwepo wa madini hayo ili kubadili maisha yao kuwa bora
zaidi.
“Naomba
nitumie fursa hii kuonesha furaha yangu ya hali ya juu baada ya wenzetu
wa GST kututhibitishia kwamba wilaya yetu ya Malinyi ina madini aina ya
dhahabu hivyo nitoe wito kwa wananchi wa Malinyi muitumie fursa hii
muhimu kuhakikisha inawanufaisha watu wa Malinyi na taifa letu kwa
ujumla,” amesema Masele.
Aidha,
Masele amewashukuru wataalamu wa GST kwa kufanya utafiti wilayani humo
na kuleta mrejesho wa utafiti walioufanya ambapo amesema uwepo wa madini
wilayani humo utasaidia kufungua fursa nyingine ikiwemo kukuwa kwa
uchumi wa kilimo na biashara mbalimbali zinazofanyika wilayani humo.
Pia,
Masele ametoa wito kwa Tume ya Madini kuhakikisha wanafungua soko la
madini na kuleta wataalamu wa madini ili waweze kuwasaidia wachimbaji
wadogo wa madini na kusaidia ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Akizungumza
kwa niaba ya Mtendaji Mkuu wa GST, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Jioloji
Maswi Solomon Mwita amesema, GST imefanya utafiti wilayani Malinyi na
kugundua uwepo wa madini ya dhahabu ambayo ni fursa kwa wawekezaji kwa
ajili ya kufanya utafiti wa kina.
Mwita
amesema GST ndiyo Taasisi inayojishughulisha na tafiti mbalimbali za
jiosayansi ikiwemo madini na kuishauri Serikali na wadau wengine wa
Sekta ya Madini namna bora ya kuendeleza rasilimali madini. Hivyo,
ameishauri Serikali ya wilaya ya Malinyi kwa kushirikiana na GST na
STAMICO kuendelea kufanya utafiti zaidi baada ya utafiti wa awali
kugundua uwepo wa madini katika eneo la Lumbanga wilayani humo.Kwa
upande wake, Mjiolojia Mwandamizi-GST, Zortosy Mpangile Maganga amesema
kuwa mwishoni mwa mwaka 2020 timu ya wataalamu kutoka GST ilifanya
utafiti wa jiolojia katika eneo la Lumbanga wilayani Malinyi ambapo
walichukua sampuli za miamba na kupelekwa katika maabara ya GST yenye
ITHIBATI ya kimataifa kwa ajili ya uchunguzi wa madini ya dhahabu lakini
pia kwa ajili ya utambuzi wa aina ya miamba iliyopo eneo hilo.
Mpangile
amesema, utafiti wa maabara ulibaini uwepo wa madini ya dhahabu yenye
kiwango cha 4.1 gramu kwa tani moja katika eneo la Lumbanga. Aidha,
matokeo ya utafiti wa jiofizikia yameonesha mipasuko katika miamba yenye
uelekeo tofauti tofauti.
Sambamba
la hilo Mpangile amesema, dhumuni la utafiti huo ilikuwa ni kukusanya
taarifa kwa ajili kutengeneza ramani za jiolojia na jiofizikia katika
maeneo ya wachimbaji wadogo wa dhahabu ili kuwasaidia kuanisha miamba ya
madini pamoja na uelekeo wake katika eneo la Lumbanga.
Kutokana
na utafiti wa jiolojia, jiofizikia na uchunguzi wa maabara, GST
inapendekeza ufanyike utafiti wa kina ili kugundua uwingi wa mashapo
katika eneo hilo.
Post A Comment: