Na  Khadija Kalili, Kibaha
MKUU wa Wilaya ya Kibaha Sara Msafiri ametoa  wito kwa wanawake wa  Mkoa wa Pwani   kuzithamini  kazi zao  mdogomdogo ambazo  ndizo zinajenga  uchumi  wa  familia    na nchi kwa ujumla  kujenga utamaduni wa kunyanyuana.

"Nawasihi  wale ambao  mnafanya biashara  ndogo ndogo kunyanyuana  kama jinsi ambavyo serikali yetu ya  awamu ya sita inavyoweka kipaumbele kwa wanawake  huku tukiwa tumepata bahati ya kuwa Rais mwanamke  Samia Suluhu Hassan kwakuwa amekuwa anazungumzia wanawake kila mahali anapokuwa "alisema  DC Msafiri.
DC alisema  hayo jana jioni  alipokuwa mgeni rasmi kwenye kongamano la wanawake lilifahamika kwa jina la 'Fursa Gala' lililowakutanisha wanawake  wa kada mbalimbali kutoka katika Wilaya za Mkuranga, Kibaha, Chalinze ,Mlandizi na Bagamoyo   lililofanyika  kwenye ukumbi wa Destiny uliopo Kwa Mathias Kibaha Mkoani  Pwani.

"Kama  Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan anavyohimiza  utalii wa ndani  na sisi tutandaa  wiki ya mjasiriamali Kibaha  Ili tuweze kupeana fursa  na ninaamini   tutaweza " alisema DC  Sara.
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Usalama Mahala pa Kazi (OSHA) Khadija  Mwenda  amesema kuwa amevutiwa na  mwitikio  wa wanawake wa Mkoa wa Pwani  jinsi walivyojitokeza  kwenye Kongamano  hilo huku akiwaahidi kurudi na kuwatembelea na kwakagua katika maeneo yao ya kazi  huku akipanga kuwapa elimu ya kutosha juu ya usalama wao  mahali pa kazi.
"Nawasisitiza kina mama kuwa makini katika maeneo yenu ya kazi kwani hakuna shughuli yote ya kiuchumi ambayo haina athari ya kiusalama wa afya mfano ni kwa watengenezaji wa batiki na sabuni na bidhaa zingine wengi hawana elimu ya usalama wa afya zao  mahala pa kazi hivyo sisi kama OSHA  tutatengeneza mpango wa kuwatembelea wajasiriamali wote tutawashauri na kwakagua" alisema Khadija.
Naye Mwanasaikolojia mbobevu aliyekuwa Mwezeshaji  Dkt. Eli Waminian  amewataka wanawake kuwekeza fikra zao katika kujiamini kwa sababu mwanamke ndiyo ngome kuu hapa duniani na dunia haiwezi kukamilika bila ya kuwepo mwanamke hivyo wajiamini katika  kilajambo wanalolifanya watafanikiwa  huku aliwataka wawe na   fikra chanya na kutoamini katika kushindwa.

"Mwanamke ni sawa na ardhi  na hii ni sayari yake hivyo wanawake waache tabia za kuwa na malalamiko, pia amewataka wanawake kuwaunganisha watoto wao na jamii kama jinsi ilivyokuwa zamani leeni watoto kwa kuwaunganisha na jamii Ili hata kama ukifa leo mtoto wako aweze kuishi maisha bila uwepo wako kwani hutoweza kyishi nae milele" alisema Dkt. Eli  ambaye amekuwa akiivutia jamii kutokana na mafundisho yake anayoyatoa kwa jamii katika makongamano mbalimbali.

Kongamano hilo limeandaliwa na Kampuni mbili ambazo ni HEROCHIC Suzana Mdonya kwa kushirikiana na Vitenge  na Tamrah Kibaha inayoongozwa na Nyamizi Yasin.


Share To:

Post A Comment: