Wakati
muendelezo wa utekelezaji mradi wa VIUNGO Zanzibar umeingia mwaka wa
wapili kamati ya ushauri ya mradi huo inakutana katika ofisi mradi huo
zilizopo mwanakwerekwe mjini Unguja.
Kamati hio ya ushauri yenye
wajumbe 20 ambao ni wakurugenzi kutoka taasisi mbali mbali za Serikali
na binafsi zinazojihusisha iwe kwa namna moja au nyengine na
utekelezwaji wa mradi huo.
Kamati hio ambayo hukutana mara nne
kwa mwaka ambapo kwa mwaka wakwanza wamekutana chini ya mwenyekiti wa
mpito Foum Ali Garu na kufanya vikao vyake vyote vilivotakiwa kwa mujibu
wa andiko la mradi huo.
Lengo kuu la kamati hio ni kutoa ushauri
kuhakikisha utekelezaji huo wa mradi unatekelezwa vizuri na kunufaisha
walengwa wote hatimae mabadiliko yaweze kuonekana kwa jamii na Taifa kwa
ujumla.
Wakati hayo yakijri katika mkutano huu wa leo wajumbe
hao wamepata Mwenyekiti mpya wa kamati hio ya ushauri ,Mohamed Khamis
Rashid ambae ni Mkurugenzi wa Idara ya kilimo Zanzibar.
Awali
mara ya kukabidhiwa nafasi hio Mwenyekiti huyo aliwataka wajumbe hao
kuhakikisha wanauelewa vyema mradi huo ili waweze kutoa ushauri wenye
tija kwa maslahi ya Taifa.
Akifungua mkutano huo Meneja mkuu wa
mradi huo Amina Ussi Khamis alisema wajumbe wa mkutano huo wanapaswa
kuwa huru na kutoa maoni yao kwani maoni hayo ndio yatakayoongeza
ufanisi ikiwemo kukuza na kuendeleza mradi huo.
Mradi huo wa
viungo unatekelezwa na Taaissi ya PDF,kwa kushirikiana na TAMWA-ZNZ
pamoja na CFP Chini ya ufadhili wa Umoja wa Ulaya kwa muda wa miaka mine
huku lengo kuu likiwa ni kuwainua wakulima wa Zanzibar kiuchumi kutoka
shehia mbali mbali za Unguja na Pemba.
Post A Comment: