Serikali imetoa Shilingi bilioni
97 kwa ajili ya kupambana na maambukizi ya TB ikiwemo kuimarisha huduma
za afya vijijini na kupata takwimu sahihi.
Hayo yamesemwa jana
na Naibu Waziri Dkt.Godwin Mollel wakati wa uzinduzi wa Muungano wa
wadau wa kupambana na kifua kikuu Tanzania ulioshirikisha wabunge,
viongozi wa dini taasisi na zingine.
Dkt. Mollel amesema Wizara
inatarajia kuwafikia watu wengi kwa kutumia magari ambayo ni Mobile
kliniki jambo ambalo linakwenda kumaliza changamoto ya ugonjwa huo na
kupeleka elimu ya moja kwa moja kwa jamii ya chini akisema lengo la
kutokomeza TB ifikapo 2030 wanaamini kuwa litafikiwa.
Aidha,
Dkt.Mollel amezungumzia Muswada wa Bima ya afya kwa wote sasa umeiva
kwani hivi karibuni ulitoka mikononi mwa kamati ya Makatibu Wakuu na
sasa unapelekwa baraza la Mawaziri ili waupitie na kuuwasilisha bungeni
Novemba mwaka huu.
Naye,Dkt.Saitole Laizer aliyemuwakilisha
Mganga Mkuu wa Serikali amesema ugonjwa huo bado ni tishio nchini ingawa
watu wengi hawajui kuwa unaua na utaendelea kuua ikiwa juhudi za
makusudi hazitachukuliwa kwa haraka.
"Vipimo vinaonyesha kati ya
watu 133,000 wanaofikiwa kwa ajili ya vipimo vya TB, 227 hukutwa na
maambukizi ya ugonjwa huo ambao kwa sasa Tanzania ina jumla ya wagonjwa
wenye TB sugu 1600 nchini kote, 400 wakigundulika mwaka jana pekee".
Amesema Dkt. Saitore
Hata hivyo ametaja changamoto ni
kutokuwafikia baadhi ya makundi yenye uhatarishi wa ugonjwa ikiwemo
watumiaji wa dawa za kulevya na wanaojidunga sindano aliosema ni
miongoni mwa makundi hatari zaidi.
“Serikali imetupatia fedha
nyingi ambazo zimefanikisha kununua magari mapya matano yatakayofanya
kazi hadi vijijini kwa ajili ya vipimo vya kwa watu wanaoshindwa kufika
hospitalini, hivyo mapambana haya yanatakiwa kuwa endelevu kwa nguvu na
kwa kila mmoja wetu,” amesema Dkt. Saitore.
Akizindua
muungano huo Spika wa bunge Job Ndugai amesema kuwa TB ni miongoni mwa
magonjwa yanayoua kwa wingi Tanzania na duniani ambayo hayatakiwi
kufanyiwa mchezo katika mapambano yake.
Spika Ndugai amewataka
Watanznaia kujihadharisha na kuchukua hatua wanapoona kuna dalili kwani
ugonjwa unaweza kumpata mtu yeyote na wakati wowote lakini akaomba
taasisi ziwekeze fedha kwa vyombo vya habari ili elimu ya ugonjwa huo
ipelekwe hadi maeneo ya vijijini.
Post A Comment: