Waziri
wa nchi ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ummy
Mwalimu akionyesha kondom aina ya safari mara baaa ya kuitoa kwenye
mashine ya kuuzia kondom kwa bei nafuu wakati wa uzinduzi wa makasha ya
kondom mjini Dodoma jana. Kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa Tayoa, Peter
Masika ambaye alisema wanatarajia kusambaza makasha 80,000 nchini.
Waziri
wa nchi ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ummy
Mwalimu akiwasili kwenye uzinduzi wa makasha ya kondom mjini Dodoma
jana. Kulia kabisa Mkurugenzi Mkuu wa Tayoa, Peter Masika ambaye alisema
wanatarajia kusambaza makasha 80,000 nchini. Mwingine ni Mbunge wa
Dodoma Mjini Antony Mavunde.
Waziri
wa nchi ofisi ya Rais tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ummy
Mwalimu akiwa kwenye picha na viongozi mbalimbali waliohudhuria uzinduzi
huo jijini Dodoma
Vijana
wa kikundi cha ngoma cha mjini Dodoma wakitumbuiza kwenye uzinduzi wa
makasha ya kusambazia kondom mjini Dodoma uliofanywa na Waziri wa
TAMISEMI, Ummy Mwalimu ambapo shirika la vijana Tayoa linatarajia
kusambaza makasha 40,000 nchi nzima.
Mkurugenzi
Mkuu wa Tayoa Peter Masika akimfafanulia jambo Waziri wa Nchi Ofisi ya
Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Ummy Mwalimu namna makasha ya
kusambazia kondom yanavyofanyakazi, mwishoni mwa wiki wakati wa
uzinduzi wa makasha hayo jijini Dodoma.
Na Mwandishi Wetu
SERIKALI
imeshauri Shirika la Vijana Tanzania (Tayoa) kusambaza makasha ya
kusambazia mipira ya kinga (kondom) na ATM za mipira hiyo kwenye
halmashauri zote 184 nchini kama sehemu ya kuchochea mapambano dhidi ya
Ukimwi.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI),
Ummy Mwalimu, amesema hayo jijini Dodoma wakati wa uzinduzi wa makasha
ya kusambazia kondom aina ya safari zinazosambazwa na Tayoa sehemu
mbalimbali nchini kupitia kampuni yake ya Vijanatz Industries Ltd .
Amesema
watu wengi wanaona haya kwenda kununua mipira hiyo madukani kwa hofu
kuwa wataonekana wahuni hivyo ubunifu wa Tayoa utasiadia watu wengi kuwa
na faragha ya kwenda kununua kinga hiyo wanapotaka kufanya mapenzi.
Amesema
angependa kuona makasha hayo na ATM hizo zinasambazwa maeneo yote
nchini ili watu wajihudumie wenyewe kwani kwa sasa baadhi ya watu
wanashindwa kwenda kuzinunu madukani kwa hofu ya kuonekana wahuni.
“Nawapongeza
Tayoa huu ni ubunifu mkubwa saba kwasababu itasaidia sana watu wengi
wanunue kondom na imekuwa mbaya sana hasa kwa wasichana kwasababu
wakinunua mipira hii ya kinga wanaonekana malaya, mimi nawashauri wakina
dada kwamba mkishindwa kujizuia kabisa kufanya ngono ni heri kuwa na
kinga kuepuka mambo mengine,” alisema Ummy
Ummy
ameongeza kuwa, shirika hilo ambalo mwakani linatimiza miaka 24
halijawahi kupoteza mwelekeo wa malengo yao tangu kuanzishwa kwake kwani
siku zote wamekuwa wakisimamia kupambana na ugonjwa wa Ukimwi ambao
alisema bado upon a unaua watu wengi hapa nchini.
“Tayoa
nawajua na tumefanyakazi nanyinyi hata kabla sijawa Naibu Waziri na
baadaye Waziri, kwa muda wote niliowafahamu nyinyi mwelekeo wenu ni
kupambana na ugonjwa wa Ukimwi hivyo nawapongeza kwa msimamo wenu
thabiti wa kupambana na janga hili,” alisema Ummy.
Waziri
Ummy aliwaomba viongozi wa serikali kwenye ngazi zote kuipa ushirikiano
taasisi hiyo itakapokuwa inasambaza mipira hiyo na kuhakikisha makasha
na ATM za mipira hiyo zinatunzwa kwaajili ya matumizi ya muda mrefu
kwenye maeneo yao.
Kwa
upande wake, Mkurugenzi wa Tayoa, Peter Masika alisema hadi sasa
wameshasambaza makasha 40,000 katika Wilaya 169 nchini na kwamba
wanatarajia kusambaza mengine 40,000 kwenye maeneo mbalimbali nchini
hivyo kufikisha 80,000.
Amesema
wanatarajia kuanza kusambaza mashine 5,000 za kutolea mipira hiyo (ATM)
katika miaka miwili ijayo na kwamba makasha watakayosambaza yana pande
mbili na yatasambazwa kwenye wilaya zote za Tanzania Bara.
Masika
aliwashukuru wafadhili wa shirika hilo ambao ni Mfuko wa Dunia wa
Kupambana na Ukimwi (Global Fund), Wizara ya Afya, Maendeleo ya
Wanawake, Jinsia na Watoto, Tume ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) na Wizara
ya TAMISEMI.
Amesema
kwa sasa Tayoa kwa kushirikiana na AMREF wanatekeleza mradi wa Global
Fund unaowalenga wasichana walio katika umri wa kubalehe na wanawake
vijana katika mikoa ya Dodoma, Morogoro, Tanga, Singida na Geita kwani
kundi hilo ndilo lililo katika hatari ya kupata maambukizi ya VVU.
Post A Comment: