Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo kulia akitiliana saini ya makubaliano  na Mhandisi wa Uzalishaji na Mauzo kutoka Kampuni ya Kahama Oils Mills Limited  Alfred Shima kushoto  kwa ajili ya usambazaji wa mabomba yenye thamani ya Milioni 419 kwa ajili ya kuhudumia miradi minne katika vijiji vinne vilivyopo kwenye wilaya za Handeni,Mkinga,Kilindi na Lushoto kulia ni Meneja wa Ruwasa wilaya ya Mkinga Mhandisi Kaijage Thomas Mzee na wengine ni watumishi wa Ruwasa mkoa wa Tanga
Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo kulia akitiliana saini ya makubaliano  na Mhandisi wa Uzalishaji na Mauzo kutoka Kampuni ya Kahama Oils Mills Limited  Alfred Shima kushoto  kwa ajili ya usambazaji wa mabomba yenye thamani ya Milioni 419 kwa ajili ya kuhudumia miradi minne katika vijiji vinne vilivyopo kwenye wilaya za Handeni,Mkinga,Kilindi na Lushoto kulia ni Meneja wa Ruwasa wilaya ya Mkinga Mhandisi Kaijage Thomas Mzee na wengine ni watumishi wa Ruwasa mkoa wa Tanga
Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo kulia akitiliana saini ya makubaliano  na Mhandisi wa Uzalishaji na Mauzo kutoka Kampuni ya Kahama Oils Mills Limited  Alfred Shima kushoto  kwa ajili ya usambazaji wa mabomba yenye thamani ya Milioni 419 kwa ajili ya kuhudumia miradi minne katika vijiji vinne vilivyopo kwenye wilaya za Handeni,Mkinga,Kilindi na Lushoto kulia ni Meneja wa Ruwasa wilaya ya Mkinga Mhandisi Kaijage Thomas Mzee na wengine ni watumishi wa Ruwasa mkoa wa Tanga
Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo katikati akionyesha waandishi wa habari makubaliano hayo yaliyoingia na Mhandisi wa Uzalishaji na Mauzo kutoka Kampuni ya Kahama Oils Mills Limited  Alfred Shima kushoto na kulia ni Meneja wa Ruwasa wilaya ya Mkinga Mhandisi Kaijage Thomas Mzee
Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo akizungumza na waandishi wa Habari mara baada ya kumalizika utiliaji wa saini makubaliano hayo


NA OSCAR ASSENGA, TANGA

WAKALA wa Usambazaji wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira Vijijini ( Ruwasa} Mkoa wa Tanga leo wameingia makubaliano na Kampuni ya  Kahama Oil Mills Limited kwa ajili ya usambazaji wa mabomba yenye thamani ya Milioni 419 kwa ajili ya kuhudumia miradi minne katika vijiji vinne vilivyopo kwenye wilaya za Handeni,Mkinga,Kilindi na Lushoto.

Halfa ya makubaliano hayo ilifanyika leo kwenye ofisi za Ruwasa zilizopo eneo la Gofu Jijini Tanga ambapo Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo aliingia makubaliano hayo na Mhandisi wa Uzalishaji na Mauzo kutoka Kampuni ya Oil Kahama Alfred Shima

Akizungumza mara baada ya makubaliano hayo Meneja wa Ruwasa Mkoa wa Tanga Mhandisi Upendo Lugongo alisema miradi hiyo ni upanuzi wa mradi wa maji eneo la Mkata wilayani Handeni,Ujenzi wa mradi mpya wa Mahezangulu wilaya ya Lushoto,Ukarabati mkubwa wa mradi wa Maji Maraba wilaya ya Mkinga na Mradi wa Maji Mafisa wilaya ya Kilindi.

Alisema miradi hiyo itakapokamilika itaongeza idadi ya watu 28,638 katika upatikanaji wa huduma watu hao ni sawa na asilimi 1 ya watu wa Tanga watakuwa wamepata hduuma ya maji safi na salama

Mhandisi Lugongo alimtaka msambazaji wa mabomba hayo kuhakikisha anayasambaza mapema na ndani ya mwezi mmoja baada ya siku 14 kutoka leo mabombo yafike kwenye miradi ili kazi ziweze kufanyika na wananchi waanza kupata huduma.

Awali akizungumza Meneja wa Ruwasa wilaya ya Mkinga Mhandisi Kaijage Thomas Mzee aliwataka wananchi kwenye maeneo ambayo mabomba hayo yanakwenda wahakikishe wanaitunza miundombinu hiyo ili lengo la mradi liweze kufikiwa.

Naye kwa upande wake Mhandisi wa Uzalishaji  na Mauzo ya Kampuni ya Kahama Mills Mhandisi Alfred Shima alihaidi wana Tanga kwamba watawapelekea mabombo yenye ubora kwa ajili ya kusambaza katika miradi hiyo.

Mwisho.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: