Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Pauline Gekul
amewaambia wachezaji wa timu ya Taifa ya Riadha kuwa macho ya Watanzania
na wapenda michezo wote yapo nyuma yao na wanamatumaini makubwa kwamba
wataiwaikilisha vyema nchi yetu.
Mhe. Gekul ameyasema hayo leo
tarehe 11 Julai, 2021 jijini Arusha wakati alipowakibidhi wachezaji wa
Timu ya Taifa ya Riadha bendera ya Taifa, vifaa vya michezo pamoja na
tiketi za ndege.
Timu ya Taifa ya Riadha ipo kambini jijini
Arusha ikijaanda na mashindano ya Olimpiki yatakayofanyika nchini Japani
mwezi Agosti, 2021.
"Macho yote ya Watanzania wapenda michezo
yapo nyuma yenu yakiwatizama na kuwafuatilia kwa karibu kwa matumaini
makubwa kwamba mtatuwakilisha vyema" - Mhe. Gekul
" Mmepata muda
wa kutosha kujifua na kujiandaa kwa zaidi ya miezi miwili, Serikali
inaimani kubwa kwamba mtarejea na medali hapa nchini" - Mhe. Gekul
Mhe.
Gekul pia amewahakikishia wachezaji hao kuwa Serikali imekuwa bega kwa
bega tangu kuanza kwa kambi na itaendelea kuiwezesha timu hiyo katika
hatua zinazofuata ili iweze kufanya vyema katika mashindano hayo makubwa
ya Kimataifa.
" Serikali imedhamiria kwa dhati kuendeleza
michezo hapa nchini, na katika kudhihirisha hilo Wizara kupitia BMT
imesaidia maandalizi ya kambi ya Timu hii pamoja na stahili nyingine za
wachezaji watakapo kuwa nchini Japani" - Mhe. Gekul.
"Lengo la
Serikali ni kuhakikisha kuwa inazisaidia Timu za Taifa pamoja na vyama
vya Michezo na Mashirikisho ili ziweze kufanya vizuri katika mashindano
mbalimbali ya Kimataifa kupitia mfuko wa Maendeleo ya Michezo
ulioanzishwa" - Mhe. Gekul
Mhe. Gekul pia amevitaka vyama pamoja
na Mashirikisho ya Michezo nchini kuzingatia utawala bora pamoja na
kuratibu mashindano katika ngazi za mikoa na Taifa ili kuibua wacheza
mahiri watakao iwakilisha nchi katika mashindano ya Kimataifa.
Timu
ya Taifa ya Riadha iko kambini jijini Arusha ikijiandaa kushiriki
mashindano ya Olimpiki nchini Japani ambapo wachezaji watatu
wamefanikiwa kufuzu viwango vya Olimpiki ambao ni Felix Simbu, Failuna
Matanga na Gabriel Geay.
Wachezaji hawa wanatarajia kuondoka nchini tarahe 27 Julai, 2021kuelekea nchini Japani kwaajili ya mashindano hayo.
Post A Comment: