Wafanyakazi kutoka Vitengo, Idara, Taasisi na Mashirika mbalimbali ya Umma na Binafsi kutoka wilaya zote za Mkoa wa Singida wakiingia kwa maandamano maalumu kwenye uwanjawa Liti,huku wakionesha mabango yenye jumbe mbalimbali zinazohusiana na siku ya wafanyakazi kwa mwaka huu.

Wafanyakazi wakifurahia Mei Day 2021.
Mkurugenzi waHalmashauri ya Ikungi Justice Kijazi akionesha cheti baada ya Halmashauri hiyo kuibuka mshindi kwa nafasi yaMwajiri Bora wa mwaka kupitia sherehe hizo. Kushotoni Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi.
Mamlaka ya Maji  Safi na Mazingira Singida (SUWASA) wakishiriki sherehe hizo kikamilifu.
Wafanyakazi wakiimba wimbo  wa Mshikamano.

Mkuu  wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi akihutubia wafanyakazi kupitia sherehe hizo zilizofanyika kwa ngazi ya mkoa.

Katibu wa TUGHE Mkoa waSingida, Ethel Kahuluda akisoma risala iliyo sheheni mafanikio, changamoto na mapendekezo ya wafanyakazi kwa niaba ya wafanyakazi wote wa mkoa.

Wafanyakazi wa Shirikalisilo la kiserikali la Maendeleo mkoani hapa SEMA wakionyesha juzi na stadi zinazotokana na matundayakazi yao, hususani kwenye eneo la karakana.

Sherehe zikiendelea
Sherehe zikiendelea
Mkurugenzi wa Ikungi Justice Kijazi (kushoto) na mmoja wa watendaji wa halmashauri hiyo wakifurahia zawadi mbalimbali walizokabidhiwa.

Wafanyakazi wakifuatilia matukio mbalimbali  kwenyesherehe hizo.

sherehe zikiendelea.
matukio mbalimbali yakiendelea.
Sherehe zikiendelea.
sherehezikiendelea
sherehezikiendelea
Wafanyakazi wakifuatilia matukio mbalimbali kwenye sherehe hizo.
Zawadi zikitolewa kwa wafanyakazi bora.
Zawadi zikiendelea kutolewa.
Mgeni rasmi wa sherehe hizo akiendelea kukabidhi zawadi kwa washindi.
Zawadi zikiendelea kutolewa.
Zawadi zikiendelea kutolewa.
Kikundi cha Ngoma na Burudani kikitumbuiza.

Maandamano yakiingia uwanjani.

Sehemu ya Itifaki ya Maandamano kuingia uwanjani.


 Singida Manispaa wakishiriki sherehe hizo kikamilifu. 



Godwin Myovela, na Dotto Mwaibale, Singida


MKUU wa Mkoa wa Singida Dkt. Rehema Nchimbi amesema tunu, fahari, tuzo na kila aina ya sifa iliyo nayo Tanzania kuanzia Awamu ya Kwanza ya uongozi wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, mpaka Awamu hii ya Sita chini Rais SamiaSuluhu Hassan, ni matunda ya kazi za wafanyakazi.

Nchimbi alitoa kauli hiyo wakati akihutubia sherehe za siku ya Mei Mosi kimkoa, mkoani hapa juzi, ambazo kwa mwaka huu zimebeba Kauli Mbinu isemayo ‘Maslahi Bora, Mishahara Juu-Kazi Iendelee.’ 

“Jeuri yote tuliyonayo kama taifa, msimamo, kujivunia kwetu, uwezo wa kuthubutu, kasi ya maendeleo na ukuaji wa Tanzania hii kiuchumi ni kwa-sababu ya wafanyakazi,” alisema.

Aliwasihi wafanyakazi kuitazama kizalendo na kuibeba kiuaminifu dhamana hiyo kubwa waliyonayo bila ya manung’uniko wala kubaguana kwa namna yoyote ile, lengo hasa ni kuongeza tija na ufanisi, ili kazi iendelee. 

“Niwaombe sana tunapoadhimisha Mei Mosi hii tukiri kwa umoja na pamoja kwamba popote alipo Rais wetu Samia na sisi wafanyakazi tupo...na tutamuunga mkono. Na katika hili naomba kila mmoja kwa nafasi na dhamana aliyonayo amfanye Rais wetu wa Awamu ya Sita aonekane,” alisisitiza Nchimbi na kuongeza:

Tunataka Mkoa wa Singida uwe ni nyumba ya amani kwa wafanyakazi na wanaofanyiwa kazi…nyumba ya furaha, usalama, na daima tuchape kazi ili kuonesha na kudhihirisha kweli sisi wafanyakazi wa mkoa huu ni watu ambao tunastahili maslahi bora, ili utumishi wa tija uendelee.

Awali akiwasilisha risala ya wafanyakazi mkoani hapa, pamoja na mafanikio kadhaa yaliyofikiwa chini ya Shirikisho la Vyama hivyo (TUCTA), Katibu wa TUGHE Mkoa wa Singida, Ethel Kahuluda, alieleza changamoto kadhaa zinazokwamisha ustawi wa wafanyakazi mahali pa kazi, ikiwemo suala la maslahi duni na kukosekana nyongeza ya mshahara.

Alisema changamoto nyingine ni kucheleweshwa kwa madai ya fedha za likizo, uhamisho, na malimbikizo ya mishahara sambamba na ucheleweshaji wa Pensheni  kwa wastaafu.

“Tunaomba serikali ilipe madeni ya watumishi kwa wakati ili kurudisha imani ya watumishi kwa serikali yao. Na suala hili la uhamishwaji watumishi tunaomba liendane na ulipwaji wa stahiki zao,” alisema Kahuluda.

Aidha, kwa niaba ya wafanyakazi mkoani hapa aliomba mamlaka husika kuzingatia kwa wakati suala la upandishaji wafanyakazi madaraja pamoja na marekebisho yake, sanjari na kupunguza kodi kwenye mishahara ili kuongeza ari ya utendaji.

Zaidi Kahuluda alipendekeza Waajiri wa Sekta Binafsi watoe mikataba ya kudumu, likizo na kima cha chini cha mishahara kizingatiwe kulingana na takwa la sheria No 5 ya Ajira na Mahusiano Kazini ya mwaka 2004.

Pendekezo lingine lililowasilishwa ni kutaka ‘Mabaraza yaWafanyakazi’ yafanyike kwa wakati na malipo ya posho yatolewe kwa mujibu wa sheria na sio kwa hisani ya wakurugenzi.

Hata hivyo, waliomba pia wafanyakazi wote wanaolipwa kwa mapato ya ndani ‘GF’ walipwe mishahara yao kwa wakati na wawekwe kwenye akiba katika Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na wapatiwe Bima ya Afya.

“Baadhi ya waajiri hawawasilishi michango ya bima ya afya kwa wakati na hivyo kupelekea waajiriwa kujigharamia ikiwa ni sawa na kulipa mara mbili,” alisema Kahuluda.

Hata hivyo, kupitia hotuba ya kitaifa ya kilele cha sherehe za wafanyakazi kwa mwaka huu iliyotolewa na Rais Samia jijini Mwanza juzi, tayari serikali imeanza kuchukua hatua za utekelezaji, ikiwemo kushusha PAYE kutoka asilimia 9 hadi 8.

Aidha Samia alisema suala la utegemezi wa ukomo wa bima ya afya kwa umri wa watoto limeongezwa kutoka miaka 18 mpaka 21, huku akiagiza madeni yote ya watumishi yaanze kulipwa.

Kuhusu makato ya HESLB aliagiza kufutwa kwa asilimia 6 ya juu na kubakiza asilimia 15 ya mshahara, huku suala la stahiki kwa watumishi wa darasa la saba waliositishiwa ajira zao lizingatiwe.

Hata hivyo kuhusu suala la nyongeza ya mshahara wafanyakazi wametakiwa kusubiri kwanza mpaka ifikapo mwezi Mei mwakani.

Share To:

Post A Comment: