Daktari Kiongozi wa Hospitali za SUA naMkuu wa idara za huduma za hospitali Dkt. Omari Kasuwi akifungua mafunzo hayo ya waelimishaji rika chuoni hapo.

Mratibu wa UKIMWI na Magonjwa sugu yasiyoambukiza SUA Dkt. Erhard Kapilima akitoa maelezo ya maengo ya mafunzo hayo kabla ya ufunguzi rasmi wa mafunzo kwa waelimishaji rika SUA.

Daktari Bingwa wa Wanawake na Uzazi ambaye pia ni Daktari kiongozi wa hospitali ya SUA upande wa Mazimbu Dkt. Elimwidimi Swai akitoa mada yake kuhusu UKIMWI na Virusivya Ukimwi VVU.

Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Watoto Dkt. Graca Chotamawe akiwasilisha mada yake kuhusu sababu  zinazochangia maambukizi ya virusi vya ukimwi na takwimu za Ugonjwa huo.

Mratibuwa UKIMWI na Magonjwa sugu yasiyoambukiza SUA Dkt. Erhard Kapilima akitoa maelezo ya malengo ya mafunzo hayo kabla ya ufunguzi rasmi wa  mafunzo kwa waelimishajirika SUA.

Washiriki wa mafunzo hayo ya uelimishaji rika wakichangia na kufuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zinawasilishwa  kwenye mafunzo hayo ya siku moja chuoni hapo. 















 Na Calvin Gwabara, Morogoro 


WANAFUNZI wa Chuo kikuu cha sokoine cha kilimo SUA waliopata nafasi ya kupata mafunzo ya uelimishaji rika chuoni hapo wametakiwa kuhakikishawana yatumia mafunzo hayo vyema kwa kutoa elimu kwa wenzao ilikusaidia kupunguza maambukizi ya Virusi vya ukimwi na magonjwa Sugu yasiyoambukiza chuoni.

Wito huo umetolewa na mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo Dkt. Omar Kasuwi ambaye ni Daktari kiongozi wa Hospitali za SUA yaliyofanyika chuoni hapo na kuwakutanisha wawakilishi wa wanafunzi kutoka kozi mbalimbali kutoka kampasi zote za SUA mkoani Morogoro.

“ Elimu hii mnayoipata nyinyi leo ya uelimishaji rika lengo lake kubwa ni nyinyi kuwa mabalozi kuhusu masuala ya ukimwi na magonjwa mengine sugu kwenyemaeneo yote mnayotoka iwe kwenye kozi zenu, mabweni yenu na hata kwenye kampasi mnazotoka ndio maana mafunzo hayo yamezingatia mchanganyiko mzuri ambao unagusa kila kona hivyo hakikisheni elimu hii mnaifikisha kwa wenzenu kokote mnakotoka ili kwapamoja tuchangie kwenye kuongeza uelewa kuhusu magonjwa haya” alisisitiza Dkt. Kasuwi.

Dkt. Kasuwi alisema kuwa pamoja na dhamira na uwekezaji mkubwa ambao unafanywa na familia na serikali katika kuwapatia vijana elimu na ujuzi ili hatimae waweze kusaidia familia na taifakwa kucnagia kwenye maendeleo lakini ndoto hizo kwa wengine hufutika kutokana na athari zamaambukizi ya VVU/UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukiza (MSY).

Aidha ameongeza kuwa pamoja na hilo lakini kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwaka 2017/2017 umeonyesha kuwa sehemu kubwa ya maambukizi mapya ya VVU yanatokea kwa vijana wenye umri kati ya miaka 15-23 kundi ambalo wengi wao wapo vyuoni na kwamba utafiti pia ulibaini wanafuinzi wa  vyuovikuu wako katika hatari zaidi ya kupata maambukizi.

Dkt. Kasuwi ameendelea kusema kuwa mwaka 2013 serikali ilifanya tathimini ili kubaini iwapo mikakati ya kudhibiti UKIMWI iliyokuwepo imeleta mafanikio yaliyokusudiwa hasa kwa watumishi wa Umma na matokeo hayo ya utafiti yalibainisha kuwa UKIMWI na MSY yalichangia sana kwenye vifo hivyo na kuathiri utendaji katika utumishi waUmma.

Daktari huyo kiongozi wa Hospitali za SUA aliesema utafiti huo ulipelekea Serikali kutoa waraka namba 2 wa mwaka 2014 uliowataka waajiri wote kuweka mikakati na kusimamia mikakati  yaudhibiti wa UKIMWI na MSY sehemu za kazi ilikupunguza athari zake.

Dkt. Kasuwi amebainisha kuwa tangu kuanza mapambano dhidi ya magonjwa hayo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo SUA kimeendelea kuwa kinara katika mipango na mikakati ya utekelezaji wa waraka na maagizo hayo ya Serikali miongoni mwa vyuo vikuu vyote nchini na ameahidi kuendelea na jitihada hizo ilikuhakikisha wanafunzi na wafanyakazi wote wanakuwa salama wakati wote ili kutimiza ndoto zao nakutimiza malengo ya kila mfanyakazi ili kuleta maendeleo.

Awali akizungumza kuhusu mafunzo hayo kwa waelimishaji rika chuoni hapo Mratibu wa UKIMWI na magonjwa sugu yasiyoambukiza SUA Dkt. Erhard Kapilima alisema sababu kuu mbili za mafunzo hayo  kwanza nikutekeleza maelekezo ya waraka huo namba mbili wa Serikali kuhusu usimamizi wa magonjwa hayo, lakini miaka michache iliyopita magonjwa hayo yameongezeka kwa kasi  nahiyo imetokana na kulegalega kwa mkazo kwenye kutoa elimu na kusimamia magonjwa hayo hivyo kufundisha waelimishaji rika kutasaidia kuongeza uelewa kwa jamii ya wanafunzi.

Ameongeza kuwa mafunzo hayo yameanza kwa jamii ya wanafunzi chuoni hapo lakini zoezi lingine kama hilo litafanyika pia kwa watumishi wa SUA watakaochaguliwa kulingana na maeneo yao ya kazi ili pia wapewe mafunzo na kupata waelimishaji rika hao kila kona ya chuo ili kuwe na nguvu ya pamoja ya kutoa elimu na kupunguza maambukizi ya magonjwa hayo na elimu kwani haiwezi kuwarahisi kutoa mafunzo kwa wanafunzi wote na wafanyakazi wote wa chuo.

Dkt. Kapilima ameongeza kuwa mafunzo hayo kwa wanafunzi yamekuwa ya kitolewa kila mwaka kwa wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wa pili  ilikusaidia kuziba pengo la wale wanaomaliza mwaka  watatu na kukifanya chuo kuendelea kuwa na waelimishaji rika wakutoka kila mwaka chuoni hapo na kusaidia mapambano ya kuyakabili magonjwa hayo.

Kwa upande wake Makamu Mwenyekiti wa SUA Heath Club, Musa Katyeka alisema kuwa mafunzo hayo yamekuwa muhimu sana kwao  kamawanafunzi kwani yamewasaidia kuwapatia wataalamuwengi wa kujitolea kutoa elimu kwa wanafunzi wenzao chuoni hapo juu ya magonjwa hayo na hivyo kuchangia kupunguza maambukizi miongoni mwao.

Kyateka ameongeza kuwa wao kama wanafunzi kila mwaka wanapata wanafunzi wengine wapya chuoni wengine wakiwa na umri mdogo hivyo ni muhimu kuwa na mafunzo ya aina hiyo ilikusaidia kupata idadi ya kutosha kuhudumia idadi kubwa ya wanafunzi wenzao kwenye mambo ya msingi ya namna ya kujikinga na maambukizi ili wawezekufikia ndoto zao na kuchangia kwenye maendeleo ya taifa.

Katika mafunzo hayo ya siku moja yaliyoandaliwa na SUA kupitia idara ya  huduma za hospitali mada mbalimbali zilifundishwa kwenye mafunzo hayo na madaktari bingwa wa magonjwa hayo pamoja na kupata shuhuda za watu mbalimbali wanaoishi na VVU mkoani Morogoro ambao nao walitapata nafasi ya kuzungumza na wanafunzi hao.


Share To:

Post A Comment: