Mwendesha
baiskeli wa kike aliongeza ladha kwenye mtindo wa hafla ya harusi baada
ya kufunga pingu za maisha na mpenzi wake katika sherehe iliyotawaliwa
na baiskeli.
Mrembo huyo ambaye pia ni fundi wa baiskeli, alifanya harusi wikendi akiwa kwenye baiskeli pamoja na waendeshaji wenzake.
Kulingana
na Sierraloaded, mrembo huyo mwenye bidii alifunga pingu za maisha na
mpenzi wake siku ya wikendi akiwa amebebwa na baiskeli.
Kawaida hafla za harusi hutawaliwa na magari, na wakati mwingine farasi lakini baiskeli ni tajira hadhimu.
Harusi
hiyo ambayo iliandaliwa Makeni nchini Sierra Leone, ilihudhuriwa na
waendeshaji baskeli ambao walijitokeza kushereheaka pamoja na mrembo
huyo ambaye ameweka rekodi kwenye nyanja hiyo nchini Sierra Leone.
Kando
na kuwa fundi wa baiskeli, Isata Sama Mondeh pia ni mwendesha baiskeli
wa kwanza wa kike kujitosa kwenye biashara hiyo ambapo amewaajiri
waendeshaji kadhaa kumfanyia kazi.
Isata,
ambaye aliwahi kushiriki mashindano ya Tour de Lunsar ambapo alinyakuwa
ushindi anapenda kuwatia moyo na kuwashauri wasichana wadogo, familia
na jamii kuhusu masuala ya tamaduni. Ushauri wake utamfaa kila mwanamke
ambaye anatazamia kuingia kwenye tasisi ya ndoa kwani si lazima utumie
magari kwenye harusi ndio uhisi kuoleka.
Via>>Tuko News
Post A Comment: