MBUNGE wa Viti Maalumu Tanzania Bara kupitia (NGOs) Mhe. Neema Lugangira katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na bodaboda wa Manispaa ya Bukoba mara baada ya kukutana na ushirika wao ili kuona changamoto ambazo wanakabiliana nazo na kuhaidi kuzifanyia kazi
MBUNGE wa Viti Maalumu Tanzania Bara kupitia (NGOs) Mhe. Neema Lugangira katikati akiteta jambo na mmoja bodaboda wa Manispaa ya Bukoba mara baada ya kukutana na ushirika wao ili kuona changamoto ambazo wanakabiliana nazo na kuhaidi kuzifanyia kazi

MBUNGE wa Viti Maalumu Tanzania Bara kupitia (NGOs) Mhe. Neema Lugangira katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na bodaboda wa Manispaa ya Bukoba mara baada ya kukutana na ushirika wao ili kuona changamoto ambazo wanakabiliana nazo na kuhaidi kuzifanyia kazi

MBUNGE wa Viti Maalumu Tanzania Bara kupitia (NGOs) Mhe. Neema Lugangira katikati akiwa kwenye picha ya pamoja na bodaboda wa Manispaa ya Bukoba mara baada ya kukutana na ushirika wao ili kuona changamoto ambazo wanakabiliana nazo na kuhaidi kuzifanyia kazi
 
MBUNGE wa Viti Maalumu Tanzania Bara kupitia (NGOs) Mhe. Neema Lugangira (Mb.) leo amekutana na Chama cha Ushirika wa Bodaboda Manispaa ya Bukoba kuwashukuru na kuwapongeza kwa namna ambavyo walishiriki katika Kampeni za Uchaguzi Mkuu 2020.

Katika utambulisho, Mwenyekiti wa Bodaboda Manispaa ya Bukoba Abdul Salum Mashankara alisema Chama hicho cha Ushirika wa Bodaboda Bukoba Manispaa kilianzishwa Septemba 30 mwaka huu chini ya usimamizi wa Mkuu wa Mkoa wa Kagera, Mhe Brigedia Jenerali Marko Gaguti wakiwa jumla ya wanachama 130.
 
 Mwenyekiti huyo aliwasilisha ombi kwa kumuomba Mbunge Neema kuungana na Mkuu wa Mkoa katika jitihada zake za kuwaunga mkono na kuwapa ushirikiano wa kimaendeleo bodaboda.

 Mwenyekiti alisema lengo la kuanzisha ushirika huo ni kutengeneza uchumi endelevu wa waendesha bodaboda wanakihusisha kupatiwa huduma ya mikopo na shughuli nyengine ikiwemo kubadilisha maisha ya wanachama wao.

Aidha alisema pia lengo ni kuwa na miradi itayotengeza ajira ikiwemo viwanda na hatimae ushirikia huu utaweza kuwasaidia kutoka kwenye utegemezi kwa leo mfano leo bodaboda waliowengi wanatumika kutokana na kwamba wana mikataba na inayowafanya kushindwa kutoka kimaisha kutokana na kutakiwa kurejedha marejesho yenye riba ya hali ya juu lakini wanakubali tu maana hawana jinsi.

“Mfano bodaboda ni sh.milion 2.6 sisi tunarejesha milioni 4.6 ndani ya miezi wastani 15 jambo ambalo limekuwa likituumiza sana “Alisema.

Kwa upande wake, Mhe Neema Lugangira (Mb.) aliwahakikishia kuwa kuja kwake ni katika jitihada zake za kumuunga mkono Mhe Mkuu wa Mkoa wa Kagera na kuwapongeza sana kwa ushindi wa kishindo wa Chama Cha Mapinduzo na aliahidi kuendelea kushirikiana nao.

Akizungumzia kuhusu changamoto ya mikataba; Mbunge Neema alisema anafikiria ni jambo ambalo atapanga siku ya kukutana na Mwenyekiti wa Bodaboda ili kuweza kupata uelewa mzuri na kuipitia mikataba waliyosaini na pengine inaweza kuwa na hoja ya kumfanya yeye aiwasilishe Bungeni kuona namna gani mnaweza kulindwa.

Mbunge Neema alisema baada ya kupata uelewa wa suala la mikataba atalifanyia kazi kwa lengo la kutafta namna ya kuwapunguzia mzigo wale ambao waliwakopeshwa pikipiki ambazo wanazitumia kwa ajili ya kujiingizia kipato kwa njia za halali na ni imani yake kubwa suluhu itakayopatikana itakuwa na msaada mkubwa kwa vijana wanaondesha bodaboda nchi nzima. 

Kama ilivyoada, Mhe Neema Lugangira (Mb.) aliongezea kuwa waendesha bodaboda ni wadau wake muhimu kwenye ajenda ya lishe bora kwa sababu wamekuwa wakiwabeba wakina mama wanapokuwa wakiwapeleka kliniki au hospitalini kupatiwa matibabu.

Alisema amedhamiria kuwajengea uwezo wa masuala la lishe bora ili pale watakapo mpakia mama na mwanae wakiwa barabarani watoa elimu ya lishe bora ili mama aelewe umuhimu wa lishe na baba aelewe umuhimu wa mama na mtoto kupata lishe bora na alisema anaamini hatua hiyo itasaidia kuhamasisha lishe bora kufanyika kwa vitendo ngazi ya kaya.

“Kwani wao kama wanaume wanaweza kuwa mabalozi wazuri kwa kushawishi wanaume wenzao ikiwemo na wao wenyewe kubeba agenda ya lishe na kuhakikisha mama mjamzito, mama mjamzito na mtoto chini ya umri wa miaka mitano anapata lishe bora maana maana mara nyingi mzigo wa lishe mnatuachia sisi wanawake nyie mnakula huko mkiwa katika mihangaiko huku wakina mama mnatuachia bajeti ndogo tunakuwa hatupati lishe ya kutosha” Alisema

 
Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: