Bi
Hilda Madeje, mkulima wa mtama katika kijiji cha Sagala B kilichopo
wilayani Kongwa mkoani Dodoma.sasa ana soko la uhakika la kuuzia magunia
30 ya mtama ambayo ni ongezeko la 70% kulinganisha na miaka ya
nyuma.Hali hii imemuwezesha kupata fedha za kutosha kujenga nyumba ya
kuishi familia yake na kulipia ada ya shule kwa watoto wake 4.
Bi
Madeje ni mmoja wa washiriki wa mradi wa majaribio wa kilimo cha mtama
wa kampuni ya bia ya TBL Plc, taasisi ya Farm to Market Alliance(FtMA)
na Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), ambao ulilenga
kuwawezesha wakulima wa mtama mbinu za kisasa za kulima zao hilo kwa
kuwapatia mbegu bora za mtama na kuongeza mavuno sambamba na
kuwahakikishia soko la uhakika la mavuno yao.
Mradi
huu wa ushirikiano ulianza mwezi Januari 2020 ambapo kampuni ya TBL Plc
ilikubali kununua mtama unaozalishwa na wakulima mkoani Dodoma, TBL
Plc, FtMa na WFP iliwasaidia wakulima hao kupata mbegu ya mtama; bima ya
mazao; itifaki za usimamizi wa zao la mtama; huduma za ugani za kilimo;
pamoja na ujumuishaji bora na soko la uhakika ili waweze kuongeza
mavuno yao.
Akizungumza
wakati wa tathmini ya msimu uliopita iliyofanyika mkoani Dodoma wiki
iliyopita, Meneja Kilimo wa TBL Plc, Joel Msechu, alisema kuwa TBL Plc
ililipa wakulima wadogo jumla ya Tzs 1.75 bilioni kwa ajili ya kununua
tani 3,000 za mtama uliozalishwa katika wilaya za Mpwapwa, Kongwa,
Kondoa, Bahi na Chamwino mkoani Dodoma, ambapo kila kilo ya mtama
ilinunuliwa kwa shilingi 550. "Mradi umekuwa na matokeo mazuri na
umewezesha kuboresha maisha ya wakulima wa mtama" aliongeza.
Kwa
mujibu wa Msechu kampuni kwa sasa inanunua asilimia 74% ya malighafi
zake nchini na imedhamiria kuongeza kiwango cha ununuzi wa malighafi
nchini katika miaka ijayo.TBL Plc imejipanga kuhakikisha inashirikiana
na wakulima wa mtama wapatao 6,000 katika msimu wa 2020-2021 ili
kukidhi kupata mahitaji yake ya tani 10,000 za mtama kwa ajili za
kuzalisha chapa zake za Eagle na Bingwa.
Akiongea
katika mkutano huo wa tathmini,Mwakilishi wa WFP, Lusajo Bukuku alisema
kabla ya kuanzishwa kwa mradi huo wakulima walikuwa wanazalisha magunia
3 hadi 4 ya mtama kwa ekari.Kutokana na kupatiwa mbinu bora za kilimo
na usimamizi mzuri mavuno yao kwa sasa yameongezeka kufikia karibu
magunia kati ya 10 hadi 11 kwa ekari.
Naye
Mwakilishi wa Farm Africa ,William Mwakyami,alisema kupitia mradi
huu,taasisi yao imesaidia kuwezesha wakulima wapatao 846 ambao
wamenufaika kwa kujiongezea kipato kutokana na kuzalisha zaidi
kulinganisha na kipindi cha nyuma kabla ya mradi na wameweza kuwa na
soko la uhakika la mavuno yao.
Kaimu
Afisa Kilimo wa Wilaya ya Kongwa, Bi Amina Msangi, amesema kabla ya
kuanzishwa kwa mradi huu wakulima walikuwa wanakabiliwa na changamoto
mbalimbali ikiwemo ukosefu wa soko la uhakika la mavuno yao. Alitoa wito
kwa wakulima kuchangamkia fursa hii ya soko la uhakika iliyopatikana
ili iwasaidie kujikwamua kimaisha.
Mpango
wa TBL Plc wa kununua malighafi nchini ni moja ya mchango wa kampuni
ambao unaenda sambamba kufanikisha jitihada za Serikali katika kukuza
uchumi wa Tanzania.
Mwaka
2018, ABInBev ilijitoa kuwapatia ujuzi, kuwaunganisha na kuwawezesha
kifedha wakulima mpaka kufikia mwaka 2025. Kutokana na mkakati huo,TBL
Plc imefanya uwekezaji wenye lengo la kuwainua wakulima wadogo nchini
Tanzania kwa kuwaanzishia huduma mbalimbali-Kilimo Uza.
Kutumiwa
meseji za simu kuwapatia taarifa mbalimbali kama hali ya hewa, taarifa
za masoko, ushauri wa kitaalamu. huduma ya mkopo wa pembejeo, mafunzo
kuhusiana na masuala ya fedha na ununuzi wa pembejeo bora na matumizi
yake, matokeo ya utafiti wa mbegu bora za mtama unaofaa kuzalishwa
nchini, mbinu za kilimo cha kisasa sambamba na kuwasaidia katika kipindi
chote cha msimu wa kilimo ili waweze kusimama na kufanya vizuri zaidi.
Post A Comment: