Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally Kakurwa (kulia) akiteta jambo na Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa (ARPP), Sisty Nyahoza wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika Ofisi ya Makao Mkuu ya Chama hicho jijini Dodoma leo.

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akielezea jambo mbele ya ugeni kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) walipomtembelea ofisini kwake wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika Ofisi ya Makao Mkuu ya Chama hicho jijini Dodoma leo. Kutoka kushoto ni Katibu wa NEC – Oganaizesheni wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Pereira Ami Silima, Mkuu wa Kitengo cha Usajili wa Vyama vya Siasa, Muhidin Mapeyo na  Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza.

Katibu wa NEC –Idara ya Oganaizesheni ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndg. Pereila Ami Silima akizungumza wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika Ofisi ya Makao Mkuu ya chama hicho jijini Dodoma leo. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) imeendesha zoezi la uhakiki ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa kukagua uhai wa vyama vya siasa nchini.

Katibu Msaidizi Mkuu Idara ya Oganaizesheni ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwangi Rajab Kundya akitoa maelezo wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika Ofisi ya Makao Mkuu ya chama hicho jijini Dodoma leo. Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) imeendesha zoezi la uhakiki ikiwa ni utaratibu wa kawaida wa kukagua uhai wa vyama vya siasa nchini.

Kutoka kushoto ni Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza,Mkuu wa Kitengo cha Usajili wa Vyama vya Siasa, Muhidin Mapeyo na Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Elimu ya Uraia toka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP), Abuu Kimario wakikagua baadhi ya nyaraka za usajili wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa siasa vyenye usajili wa kudumu katika ofisi za Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dodoma.

Mkuu wa Kitengo cha Sheria wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Goodluck Mwangomango akifafanua jambo mbele ya ujumbe kutoka Ofisi ya Masjili wa Vyama vya Siasa (ORPP) wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika ofisi za Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dodoma.Kushoto ni Afisa Tehama wa CCM, Magoti Marwa na kulia ni Katibu Msaidizi Mkuu – Idara ya Mambo ya Siasa na Uhusiano wa Kimataifa wa CCM, Christopher Magala.

Katibu Msaidi Mkuu – Idara ya Uchumi na Fedha, Victor Septemba Patrick akifafanua jambo mbele ya ujumbe kutoka Ofisi ya Masjili wa Vyama vya Siasa (ORPP) wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika ofisi za Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akionyesha hati za usajili na bodi ya wadhamini za CCM wakati wa zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika ofisi za Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dodoma. Kanuni za Sheria ya Usajili wa Vyama vya Siasa ya Mwaka 2019 inataka hati hizo kutundikwa ukutani katika ofisi za vyama hivyo.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. Bashiru Ally Kakurwa akielezea jambo wajumbe kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa (ORPP) MARA mara baada ya kumaliza zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika ofisi za Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dodoma.

Msajili Msaidizi wa Vyama vya Siasa (ARPP), Sisty Nyahoza akifurahia jambo na Waziri Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Nne na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Mhe. Mizengo Pinda walipokutana katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM jijini Dodoma leo walipofika katika ofisi hizo kwa ajili ya zoezi la uhakiki wa uhai wa vyama vya siasa vyenye usajili wa kudumu katika ofisi za Makao Makuu ya chama hicho leo jijini Dodoma. (Picha na Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa).
Share To:

msumbanews

Post A Comment: