Mafundi wa shirika la lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Mufindi na Kilolo mkoani Iringa wakionesha mask (barakoa ) walizotengeneza kwa kutumia vitambaa ambazo ni bora zaidi na unaweza kuzifua
...........................................
KATIKA kukabiliana na changamoto ya uhaba wa Mask (barakoa)mitaani shirika la lisilo la kiserikali la Rural Development Organization (RDO) Mufindi na Kilolo mkoani Iringa limeanzisha utengenezaji wa barakoa hizo ili kusaidia jamii kujinginga na maambukizi ya virusi vya Corona mkoani hapo na nje ya mkoa .
Akizungumza jana waandishi wa habari mkurugenzi wa shirika RDO Fidelis Filipatali alisema kuwa wamelazimika kuanzisha utengenezaji wa barakoa baada ya kuona uhitaji wa barakoa ni mkubwa na upatikanaji wake ni mgumu na hata kama zinapatikana gharama yake ni kubwa ambayo wananchi wenye uchumi wa chini na wale wasio na kipato wamekuwa wakishindwa kumudu gharama ya kununua barakoa hizo .
Hivyo alisema wamefanikiwa kubuni barakoa za kisasa za kujinginga na gonjwa la Covid 19 ,barakoa ambazo unaweza kuzitumia kwa muda mrefu zaidi bila kuzitupa maana hizo ambazo wanazitengeneza wamezitengeneza kwa ubora zaidi na mtumiaji anaweza kuzifua mara kwa mara na kuzitumia tena pasipo tatizo lolote .
Filipatali alisema shirika hilo limekuwa likizitengeneza barakoa hizo kwa kuwatumia watoto ambao wanatoka katika mazingira magumu ambao wamekuwa wakifundishwa ufundi mbali mbali kupitia chuo chake kilichopo Mdabulo , Mafinga na Kilolo japo kiwanda cha kutengeneza barakoa hizo kipo mjini Mafinga .
" TUnachohitaji kuwezeshwa kupata vitambaa vya kutosha na vifaa zingine kwa ajili ya kutengenezea barakoa hizi na kama tutawezeshwa tunao uwezo wa kuzalisha barakoa kwa wingi na kuzigawa bure ama kwa kuziua kwa gharama ndogo zaidi kwenye taasisi mbali mbali na wananchi wa vijijini na mijini wenye kipato cha chini ili waweze kuzitumia kujikinga na maambukizi ya virusi hivi hatari vya Corona " alisema
Kwa sasa wameweza kutengeneza barakoa kwa ajili ya matumizi ya shirika hilo badala ya kuhangaika kununua madukani kwa gharama kubwa ya shilingi 15000 kwa barakoa ya bei ya juu ambayo unaweza kutumia kwa siku mbili wao wanatengeneza wenyewe barako za kisasa zaidi za kutumia hata kwa miezi mitatu na kuendelea pasipo kupoteza ubora wake .
Hata hivyo alisema kuwa RDO kupitia vyuo vyake vya vya ufundi stadi wameendelea jihusisha na kutoa mafunzo ya ufundi stadi kwa vijana hasa waliopo vijijini kwa lengo la kuwawezesha kupata ujuzi mbalimbali wa mafunzo ya Ufundi Stadi ili waweze kuendana na sera ya uchumi wa viwanda kwa kuongeza idadi ya watu kujitegemea wao wenyewe, familia zao, jamii inayowazunguka na taifa kwa ujumla kwa kujiajiri wao wenyewe na kuajiriwa nakwa kupitia gonjwa hilo la Covid 19 wameendelea kubuni mbinu ya kujikinga na kuwakinga wananchi na virusi vya Corona .
Alisema ubunifu mbali mbali wanaoufanya unapelekea vijana zaidi ya 300 kupenda kuishi mazingira ya vijijini na kuto kimbilia mijini na nchi za nje badala yake wanaweza kujiajiri wenyewe huko huko vijijini kupitia fani mbali mbali walizopewa .
Hata hivyo pamoja na kubuni kutengeza barakoa alisema chuo kabla ya kufungwa kwake kwa agizo la serikali kutokana na janga la Corona walikuwa na fani mbali mbali zinatolewa kwa muda mrefu (miaka 3) na muda mfupi (miezi 3 na 6) ni umeme wa majumbani na Viwandani (Electrical Installations), Nishati Jadidifu (Renewable Energy) Uungaji na Uundaji Vyuma (Welding and Metal
Fabrications),Upishi (Food Productions), Useremala (Carpentry and Joinery), Mitindo na Ushonaji (Design, Sewing and Cloth Technology), Ufugaji (Animal Husbandry), Uwashi(Masonry and Bricklaying), Mabomba (Plumbing and Pipe Fitting) na Kompyuta (Computer Applications).
Fabrications),Upishi (Food Productions), Useremala (Carpentry and Joinery), Mitindo na Ushonaji (Design, Sewing and Cloth Technology), Ufugaji (Animal Husbandry), Uwashi(Masonry and Bricklaying), Mabomba (Plumbing and Pipe Fitting) na Kompyuta (Computer Applications).
MWISHO
Post A Comment: