Mganga mkuu wa mkoa wa Iringa Dkt Salim Robart akifungua warsha kwa niaba ya Ras Iringa
.
Baadhi ya washiriki wa kikao hicho
Mratibu wa mradi Tanzania Gabriele Maneo
.....................
SERIKALI ya mkoa wa Iringa imepongeza jitihada mbali mbali zinazofanywa na shirika lisilo la kiserikali la CUAMM ,CEFA na MAWAKI kwa jitihada za kusaidia kutokomeza utapiamlo na udumavu katika mkoa kupitia mradi wake wa Nourishing the Future.
Pongezi hizo zimetolewa leo mjini Iringa na katibu tawala wa mkoa wa Iringa Happines Seneda ambae alisema kuwa mashirika hayo yaliyopo chini ya waziri mkuu wa Italia kwa kazi nzuri ya kusaidia jamii ya mkoa wa Iringa kupitia mradi wa Nourishing the Future kupunguza tatizo la utapiamlo na udumavu kwa watoto jambo ambalo ni jema kwa mkoa na Taifa
alisema itihada hizo za kuanzisha mradi wa Nourishing the Future katika mkoa wa Iringa kwenye halmashauri za Kilolo na Mufindi zitasaidia kwa kiasi kikubwa kwenda na kasi ya uongozi wa mkoa katika mapambano dhidi ya vita ya kutokomeza utapiamlo na kupunguza udumavu kwa watoto chini ya miaka mitano kutoka asilimia 47 iliyopo sasa na kushusha zaidi kiwango hicho cha udumavu ndani ya mkoa .
Seneda alisema mradi huo wa Nourishing the future utakaotekelezwa katika wilaya mbili za Mufindi na Kilolo ndani ya mkoa wa Iringa ,kuwa ushirikiano mzuri ambao CUAMM na MAWAKI wameonesha ndani ya mkoa kupitia Halmashauri zake ni ushirikiano wa kupongezwa kwani mradi huo jumuishi unahusisha kilimo,afya na lishe umekuja wakati ambao mkoa upo katika utekelezaji wa mkabata wa kupunguza udumavu .
" Ni matumaini yangu kuwa mradi utasaidia kuboresha siku 1000 za kwanza za uhai wa mtoto pia tunategemea matokeo mazuri hasa katika kiashiria cha udumavu ambacho ni asilimia 47 isiyokubalika kimkoa ,ninaomba nikazie utekelezaji wa malengo mahususi ya mradi ambayo ni kuongeza uwiano wa watu wanaotumia mlo wenye mchanganyiko ambapo kwa sasa hali halisi kwa watoto ni asilimia 25 tu ndio wanapata mlo wenye mchanganyiko wa vyakula mbali mbali " alisema
kupunguza kiwango cha udumavu kwa watoto ,kuboresha hali ya lishe na afya kwa jamii iliyo katika mazingira hatarishi kwani kwa kufanya hivyo kutasaidia kwa kiasi kikubwa kuwa na jamii yenye afya bora isziyokuwa nautapiamlo wala udumavu .
Hivyo aliwaomba wadau hao wa CEFA kufanya utafiti wa awali ili kujua hali halisi ilivyo katika maeneo hayo ya utekelezaji wa maradi huo pia jamii ihamasishwe katika uzalishaji na utumiaji wa mazao ya kilimo na mifugo yenye viini lishe kwa wingi ili kuboresha hali ya lishe na uchumi wa kaya.
" Suala la lishe ni mtambuka ninaomba tushirikiane vema kulitekeleza ,ushirikishwaji katika mradi uratibiwe kuanzia ngazi ya mkoa hadi vijiji na mitaa na takwimu zikusanywe vema ,zichambuliwe na zitumike katika kufanya maamuzi na tathimini za utekelezaji zifanyike ili kujua maendeleo ya mradi na endapo malengo yanafikiwa niwahakikishie tu wadau wetu kwamba sisi kama serikali tupo tayari kufanya kazi na ninyi na tunawakaribisha sana endapo mtapata changamoto yoyote ya kiutendaji tuwasiliane ili kuitatua haraka kabla ya kuathiri utendaji kazi wenu "
Aidha aliwataka watendaji wa mamlaka za wilaya kuratibu vema na kusimamia afua za sekta mbali mbali ili ziweze kuonesha matokeo chanya kama ambavyo serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dkt John Magufuli inavyoendelea kupigania maendeleo mbali mbali katika Taifa .
Hivyo aliomba mradi huo wa Nourishing the Future kusaidia katika kupunguza udumavu na kuboresha hali ya ulishaji /ulaji wa vyakula mchanganyiko kama ilivyooneshwa katika malengo mahususi ya mradi huo.
Meneja wa wa mradi wa CEFA Giovanni Spata alisema kuwa wao kama wadau wa maendeleo nchini wamekuwa bega kwa bega na serikali ya Tanzania katika kushiriki kuchangia miradi mbali mbali ya kimaendeleo katika maeneo ambayo mradi wao unafanya kazi na wataendelea kufanya hivyo kwani ni moja kati ya malengo ya miradi yao kusaidiana na serikali kuwaletea wananchi maendeleo .
Alisema kuwa tayari wamekwisha fanya utafiti kwawilaya zote ambazo mradi huo utafanya kazi na wanajua wanashughulika na watoto wangapi wenye udumavu na utapiamlo hivyo wanapoanza utekelezaji wa mradi huo wanaamini kabisa walengwa watafikiwa na kunufaika zaidi na mradi huo .
Awali mratibu wa mradi huo wa CEFA Tanzania Gabriele Maneo alisema kuwa mradi huo utafanya kazi katika kata tatu za Halmashauri ya Iringa ambazo ni Mgama ,Maboga na Kihanga wakati wilaya ya Kilolo mradi utafanya kazi katika kata tano za Dabaga Idete , boma la Ng'ombe,Mtitu na Ng'ang'ange huku wilaya ya Mufindi mradi utafanya kazi katika kata tatu za Mpanda ,Kasanga na Igombavanu kuwa jumla ya vijiji vitakavyofikiwa na mradi huo ni vijji 45 kwa maeneo yote
Maneo alisema utekelezaji wa mradi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza utapiamlo na udumavu katika vijiji vyote vya mradi huo pamoja na kuwawezesha wananchi kuongeza kasi ya uzalishaji wa mazao mbali mbali ya chakula ,ufugaji ,elimu na afya
Post A Comment: