Mkuu wa wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Asia Abdallah akijiandaa kutimua mbio wakati akikagua mradi wa ufugaji nyuki kijiji cha Lulindi kata ya Ukwega baada ya nyuki kuwajeruhi watu watatu wakiwemo waandishi wawili wakati akikagua mradi huo
Waandishi wa habari na wananchi wakimbia baada ya kushambuliwa na nyuki
Mkuu wa wilaya ya Kilolo na msafara wake wakianza ukaguzi wa mradi wa ufugaji nyuki kabla ya nyuki kuwafukuza
...................................................................
MKUU wa wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Asia Abdallah na msafara wake walazimika kutimua mbio na kuahirisha zoezi la ukaguzi wa mradi wa ufugaji wa nyuki kijiji cha Lulindi kata ya Ukwega baada ya kushambuliwa na nyuki Mwandishi Francis Godwin anaripoti toka Kilolo
Tukio hilo lilitokea majira ya saa 6 mchana baada ya mkuu huyo wa wilaya na msafara wake kutembelea mradi wa kijiji wa ufugaji nyuki kwa ajili ya kukagua mradi huo wenye mizinga zaidi 92 .
nameagiza viongozi wa serikali za vijiji vya kata ya Ukwega kuhamasisha wananchi kufunga nyuki na kulima kupanda Parachichi kama mazao yao ya kiuchumi
Akizungumza wakati wa mikutano yake ya hadhara ya kuhamasisha maendeleo katika vijiji vya Lulindi ,Ipalamwa ,Ukwega ,mkalanga na Makungu kata hiyo ya Ukwega mkuu huyu alisema serikali haipendi kuona watu wake ni masikini wa kipato hivyo inapambana kuwawezesha kiuchumi zaidi .
Alisema Rais Dkt John Magufuli toka aingie madarakani amejipambanua kuwa ni Rais wa wanyonge na kazi kubwa anayoifanya ni kuona watanzania wote wananufaika na raslimali ya Taifa kupitia sera ya viwanda .
Kwani alisema ufugaji wa nyuki wenye tija na kilimo cha mazao ya biashara kama Parachichi na mazao mengine yatawezesha wananchi kukuza kipato chao .
Asia alisema viongozi wa serikali za vijiji hadi wao wa wilaya wanapaswa kufanya kazi ya kuwasaidia wananchi kuondokana na umasikini kama ambavyo kwa upande wake na viongozi wa wilaya hiyo wanavyofanya kuwafikia wananchi .
Kuhusu Kero ya maji kijijini hapo alisema atahakikisha anashirikiana na viongozi wa wilaya hiyo kuhakikisha wananchi wanapata huduma ya maji safi na salama .
Aidha alisema ili maendeleo yaweze kufanyika asingependa kuona kuna watu ambao hawafanyi kazi na kuagiza viongozi wa vijiji kuwabana wote wanaoshinda vijiweni hasa vijana pia kuwawajibisha kisheria wanawake wanaokwenda kunywa pombe na watoto ama wale wenye ujauzito .
Pamoja na kuagiza kukamatwa kwa wanawake hao watakaokutwa katika maeneo ya starehe usiku pia mkuu huyo wa wilaya ameagiza kukamatwa kwa vijana wote wanaoshinda vijiweni wakipiga porojo pasipo kwenda shamba kufanya shughuli za uzalishaji mali .
Alisema haiwezekani viongozi wa serikali za vijiji kuendelea kuwafumbia macho wanawake wenye tabia ya kukaribisha udumavu kwa watoto wao kwa kuwanywesha pombe watoto wadogo ama kuona wanawake wajawazito ambao kimsingi wanatakiwa kutunza mtoto aliyepo tumbuni kwa kula vyakula vinavyohitajika kwa ajili ya afya ya mtoto aliyepo tumboni wakaachwa wakinywa pombe usiku kucha .
"Wewe mwanamke una mtoto mdogo ama una ujauzito kwenye pombe usiku unatafuta nini tena nimeambiwa kuwa wanawake wanaokwenda wa watoto wachanga kwenye pombe wakiona wana mambo yao ambayo yanazuia kwenda na mtoto wamekuwa wakimnywesha ulanzi ama pombe kali mtoto ili alale usingizi na yeye aendelee na starehe zake vichakani nasema sitakubali kuona watoto wakihatarishiwa afya zao kwa kuendelea kunyweshwa pombe nasema kamateni wote na wapigeni faini ili faini hizo zifanye kazi za kimaendeleo katika vijiji " alisema Asia
Kuwa hajazuia wanawake hao kunywa pombe ila amezuia wanawake wenye watoto na wajawazito kukutwa kwenye pombe majira ya usiku na kama wanatamani pombe basi ni vizuri wakanunua na kwenda kunywa nyumbani wakati wakiwaandalia watoto chakula ila sio kugeuza pombe na chakula kwa watoto .
Post A Comment: