Mbunge wa jimbo l Segerea Bonah Ladslaus akizungumza na wananchi wa Segerea wakati wa ziara yake .
Mbunge wa Segerea ,Bonah Ladslaus akiangalia maji mto Msimbazi Kata ya Segerea Manispaa ya IlalaPicha na habari na Heri Shaaban
MBUNGE wa Segerea Bonnah Kamoli amewataka Wananchi wa jimbo la Segerea kushirikiana na Wenyeviti wa Serikali za Mitaa katika kuleta Maendeleo Jimboni humo.
Bonnah aliyasema hayo Kata ya Segerea mtaa wa Segerea Manispaa ya Ilala Leo, alipokwenda katika ziara ya kutatua kero za wananchi.
" Wananchi wenzangu wa Jimbo la Segerea nawaomba tuwatumie Wenyeviti wetu vizuri Katika kuleta Maendeleo ya mitaa yenu.
"Segerea tuna wenyeviti wa Mitaa 61, mkiwatumia vizuri maendeleo yatakuja kwa kasi" alisema Mh.Bonnah .
Kamoli aliongeza kuwa Jimbo La Segerea lina Kata 13 Mitaa 61 na wakazi milioni 1.4. ni jimbo la kwanza kuwa na wakazi wengi nchini na pia Kata inayoongoza kwa kuwa na wakazi wengi nchini Tanzania iko jimboni kwetu kata ya Vingunguti.
Aliwataka wananchi tukiwatumia wenyeviti vizuri kuwasilisha taarifa za kero zao ili ziweze kufika Ofisi ya Mbunge mapema pamoja na ofisi zingine za serikali kwa ajili ya kuzitatua.
Alisema Jimbo hilo ni kubwa linataka ushirikiano katika kuleta Maendeleo.
Alisema katika jambo la maendeleo ushirikiano lazima kuwasilishe kero serikali za mitaa pamoja na kushiriki vikao vya kuleta Maendeleo.
" Mimi kwa nafasi yangu nipo tayari kushirikiana na wenyeviti wote muda wote masaa yote 24 ,mmenichagua ili niwatumikie".
Aidha katika ziara hiyo mbunge amehaidi kupeleka kifusi cha kokoto na mawe kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya eneo lililoharibiwa na maji ili kuweza kurudisha mawasiliano katika barabara ya mtaa wa Segerea na Migombani.
Wakati huo huo Mbunge Bonnah amewataka wakazi wa Mtaa wa Segerea ambao hawana Maji safi na Salama ya DAWASA kufika Ofisi ya serikali za mitaa kwa ajili ya kuorodhesha majina yao ili wapeleke maombi yao DAWASA ili waunganishwe Maji.
Post A Comment: