Rais Magufuli amempigia simu rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Ado Novemba na kumwambia anafuatilia shughuli hiyo ya kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere.

Kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere linafanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaaam.

"Nakusikiliza usiwe na wasiwasi na maagizo yangu niliyoyatoa Waziri Mkuu atayawasilisha hapo kwenu, ninawapenda sana, wasanii oyeeee," alisema Rais Magufuli.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika Kongamano hilo.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: