Rais Magufuli jana ametembelea Hifadhi ya Taifa ya Katavi na kisha kuzungumza na Maafisa na Askari Wanyamapori wa Shirika la Hifadhi za Taifa (TANAPA) ambapo amewapongeza kwa kazi nzuri ya kuhifadhi wanyamapori ikiwemo kukabiliana na ujangili hali iliyowezesha kuongezeka kwa idadi ya wanyama wakiwemo wale waliokuwa hatarini kutoweka lakini amewasihi wachache miongoni mwao ambao wanashirikiana na wahalifu waache tabia hiyo.

“Wapo wenzenu wachache wanaoshirikiana na majambazi, waache na wakipatikana wa namna hiyo, peleka mahakamani wafunguliwe kesi ya uhujumu uchumi," amesema Rais Magufuli.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia wanyama aina ya viboko katika hifadhi ya Taifa ya Katavi  mara baada ya kusimama wakati akielekea Mpanda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akichagua nyama ya porini mara baada ya kujumuika na wadau mbalimbali, Wafanyakazi wa TANAPA, Askari wa Wanyama Pori, Wabunge, Mawaziri katika mbuga ya wanyama ya Katavi wakati akielekea Mpanda mkoani Katavi.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: