Mpendwa
msomaji wetu, Maada yetu nyingine ya leo ni mbinu za kupanga
jinsia ya mtoto wa kuzaa kabla mkeo hajashika mimba....
Siku hizi ulimwengu umeendelea sana, matatizo mengi yanatibika kwa msaada wa wataalamu...Hakuna tena haja ya kupigana na kupeana talaka kisa jinsia ya mtoto...
Somo letu la leo litajikita zaidi katika mbinu za kuzaa mtoto wa kike.
Ni vipi jinsia ya mtoto huainishwa?
Siku hizi ulimwengu umeendelea sana, matatizo mengi yanatibika kwa msaada wa wataalamu...Hakuna tena haja ya kupigana na kupeana talaka kisa jinsia ya mtoto...
Somo letu la leo litajikita zaidi katika mbinu za kuzaa mtoto wa kike.
Ni vipi jinsia ya mtoto huainishwa?
Kinyume
na wengi wanavyofikiria kwamba mwanamke au mwili wa mwanamke ndio wenye
jukumu la kuainisha jinsia ya mtoto kwa kuwa yeye ndiye anayebeba
mimba, uhakika wa mambo ni kuwa mwanamume ndie mwenye uwezo wa kuainisha
jinsia.
Kila
yai la mwanamke lina chromozomu mbili za X. Iwapo manii ya mwanamume au
spemu(ambayo ina chromozomu X na Y) itakuwa na X na kurutubisha yai la
mwanamke lenye X tupu, basi mtoto atakayezaliwa atakuwa mwanamke.
Vilevile iwapo spemu ya mwanaume itakuwa na Y na kurutubisha yai la mwanamke lenye X, basi mtoto atakayezaliwaatakuwa mwanamume.
Hivyo
kwa kufahamu suala hilo, ni matumaini yetu kuwa vile visa vya kinamama
kuachwa eti kwa kuwa hawakuzaa watoto wa kiume au wa kike vitapungua
katika jamii zetu. Mke wako asipozaa mtoto wa jinsia uitakayo, usifikiri
kuwa yeye ndiomwenye makosa.
Wakati
mwanamume anapomwaga mbegu, spemu kati ya milioni 200 hadi 400 humwagwa
katika uke wa mwanamke. Baadhi ya spemu hizo huwa zina chromozomu X na
baadhi zina chromozomu Y.
Hata hivyo, ni spemu moja tu ambayo hutakiwa kwa ajili ya kurutubisha yai la mwanamke nakuunda mimba.
Nadharia
mbalimbali zinazotolewa kwa ajili ya kusaidia kuchagua ni jinsia gani
unaitaka awe nayo mwanao, zinategemea suala la kuandaa mazingira katika
uke na mwili wa mwanamume na mwanamke,yatakayosaidia spemu ya baba yenye
chromozomu inayotakiwa irutubishe yai la mama, na hivyo kutungwa mimba
ya jinsia inayotakiwa.
Njia ya Dr. Shettles ya kuzaa mtoto wa kike
Njia hii imekuwa ikitumiwa na watu wengi kwa miaka mingi sana na imewasaidia kuweza kuzaa mtoto wa kike.
Wengi
wanasema kuwa uwezekano wa kufanikiwa njia hii ni asilimia 90. Njia ya
Dr. Shettles inategemea msingi kwamba, chromozomu Y (yenye kuwezesha
kutungwa mimba ya mtoto wa kiume) ni ndogo na yenye kwenda kwa kasi
zaidi ikilinganishwa na chromozomu X(yenye kuwezesha kutungwa mimba ya
mtoto wa kike) ambayo ni kubwa na huenda polepole.
Pia
kwa kutegemea kuwa chromozomu X inaishi muda mrefu zaidi kuliko ile ya
Y.Hivyo Dr. Shettles anashauri kuwa iwapo unataka kuzaa mtoto wakike
uhakikishe kuwa:
1.Unajamiiana
siku 2 au 3 kabla ya Ovulation. Kinadharia spemu za kiume zitakuwa
zimeshakufa hadi kufikia siku hasa ya Ovulation na kuziacha spemu za
kike zikiwa hai tayari kurutubisha yai na kuunda mtotowa kike.
2.Anashauri
pia wanawake wajizuie kufikia kileleni (orgasm) kwani hali hiyo
itaufanya uke uwe na hali ya asidi ambayo ni kwa faida ya spemu ya kike
yenye chromozomu X.
3.Pia
anawashauri wazazi wanapojamiina wawe katika haliya mwanamke kulala
chini na mwanamume juu au missionary position. Kwani anasema kuwa mtindo
huo huziwezesha spemu zenye chromozamu X zimwagike karibu na mlango wa
uke na kuwa na uwezekano mkubwa wa kuingia ukeni na kutungwa mimba.
Kuna wengine wanaamini kwamba baadhi ya lishe na vyakula vya aina mbalimbali husaidia kutunga mimba ya mtoto wa kike.
Kwa
mfano kuna wanaoamini kuwa kula baadhi ya vyakula huufanya uke uwe na
hali ya asidi ambayo husaidia Chromozomu Y ife katika uke.
Nadharia
nyingineyo inayotumiwa katika kuchagua jinsia ya mtoto inasema
kwamba,mwanamke anayetaka kubeba mimba ya mtoto wa kike ale vidonge vya
virutubisho (supplements) vya Calcium na Magnessium mwezi mmoja kablaya
kubebea mimba.
Iwapo unataka kutumia vidonge vya virutubisho ili uweze beba mimba ya mtoto wa kike, ni bora ushauriane na daktari wako kwanza.
Hii ni kwa sababu dawa hizo huweza kuingiliana na dawa nyinginezo za magonjwa mbalimbali.
Baadhi ya vyakula vinavyotajwa kuwa vinasaidia katika kutunga mimba ya mtoto wa kike ni.
-->>>Mahindi, nyama, maharagwe, samaki, tunda damu, mayai na maini.
Vyakula
hivyo ni vya asidi hivyo huifanya PH ya mwili wako hupungua na kuwa ya
acidi. Hali hiyo husaidia kuua spemu za Y na hivyo kusaidia kuzifanya
spemu za X ziwe na uwezekano mkubwa wa kurutubisha yai.
Hivyo
mwanamke anayependelea kubebea mimba ya mtoto wa kike anashauriwa
kutokula vyakula vyenye alikali ambavyo ni kama, ndizi, chokleti, juisi
ya machungwa, viazi, tikiti maji na vinginevyo.
Post A Comment: