Na Andrew Chale, Zanzibar

TAMASHA la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) la 22 kwa mwaka huu leo limeendesha mafunzo kwa Watoto wenye tatizo la Down Syndrome ama Watoto mfanano kama wanavyojulikana visiwani hapa.

Mafunzo hayo yanayotolewa na ZIFF  kwa kushirikiana na taasisi ya kutoka Uholanzi ya Media Lab ambayo imekuwa ikitoa mafunzo kwa watoto mbalimbali visiwnai hapa kwa kutumia teknolojia kwa masuala ya sanaa ikiwemo utengenezaji wa vikatuni, Uigizaji, utangazaji, uandishi wa habari, kuchora na mambo mengine katika masuala ya Sanaa.

Kwa mujibu wa Mratibu wa Warsha za ZIFF 2019, Ahmed Harith amebainisha kuwa, mafunzo hayo  ni ya mara ya kwanza kwa ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kati ambapo wanatarajia Watoto zaidi ya 1,000 kushiriki mafunzo hayo.

“Mafunzo haya yanatolewa kila siku kuanzia Julai 5 na yataisha mpaka mwisho wa tamasha. Ambapo kwa siku watoto zaidi ya 100 wanapata kushiriki.

Watoto hao wanatoka shule mbalimbali za visiwani hapa na baadhi yao nje ya skuli” alisema Ahmed Harith.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Taasisi ya Down syndrome Initiative Zanzibar, Bi. Ahlam Abdalla Azzam  amelipongeza tamasha la ZIFF 2019 kwa kuwakumbuka watoto hao ambao wameweza kujifunza mambo mbalimbali kama watoto wengine licha ya uelewa wao kuwa mdogo.

“Tunaipongeza ZIFF kwa kuwajali watoto Mfanano wameweza kujifunza vitu vingi ikiwemo kuimba, kucheza na kufanya vitu vya ubunifu.

Pia wameweza kujfunza namna ya kuchora michoro na na kutengeneza vikatuni kupitia program za kisasa za teknolojia ya Media Lab” alieleza Bi. Ahlam Abdalla Azzam.

Zanzibar inaelezwa kuwa na Watoto wengi wenye tatizo la Down Syndrome ambapo Serikali na wadau wamekuwa wakichukua hatua za kuwasaidia watoto hao.

Mwisho.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: