Waziri wa Mifugo na Uvuvi Luhaga Mpina akizungumza katika kilele cha wiki ya maziwa duniani ambapo kitaifa imefanyika mkoani Arusha.

Waziri wa Mifugo Mhe.Luhaga Mpina akiwa na mkuu wa wilaya ya Arusha Mhe.Gabriel Daqqaro katika kilele cha siku ya maziwa duniani iliyoadhimishwa kitaifa mkoani Arusha.
 Wanafunzi wakiwa katika Fokeni ya kugawiwa maziwa leo katikabuwanja wa Shekhe Amri Abeid ambapo ni kilele cha siku ya maziwa duniani iliyoadhimishwa kitaifa mkoani Arusha.
 Wanafunzi wakinywa zao maziwa kama wanavyoonekana katika picha
Mara baada ya kugawiwa maziwa leo katika uwanja wa Shekhe Amri Abeid ambapo ni kilele cha siku ya maziwa duniani iliyoadhimishwa kitaifa mkoani Arusha.

Na.Vero Ignatus Arusha.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi amefunga Maadhimisho ya 22 ya kilele cha wiki ya maziwa duniani ambapo kitaifa yamefanyika mkoani Arusha  yenye kauli mbiu isemayo maziwa yaliyosindikwa kwa afya na buchumi wa viwanda"

Katika sherehe hizo zaidi ya lita za maziwa 5810 zimekusanywa na wadau wa maziwa na kugawa kwa wanafunzi wa shule za msingi,wasiojiweza na katika mahosipitali katika mkoa wa Arusha bure.

Mhe.Mpina amesema  unywaji wa maziwa ni swala muhimu na nyeti katika maisha ya kila siku ya mwanadamu,ambapo amesema Taifa la Tanzania lina zaidi ya mifugo asilimia 60% na ni nchi ya pili Afrika kwa kuwa na mifugo mingi  lakini uzalishaji wake wa maziwa ni duni

"Ukilinganisha uzalishaji wetu hapa nchini haulingani na baadhi ya majirani zetu kwani sisi lita bil 2.2 ambapo sisi tunayomaeneo mazuri ya malisho tofauti na wenzetu,Kenya lita bil.5.6,uganda lita 2.7

Amesema serikali mwaka jana 2018  waliweza kukamata jumla ya lita tani 26.5 za maziwa na nyama ambazo zilijaribu kuingia nchini bila kufuata sheria na utaratibu, amesema Serikali imeendelea kuimarisha mipaka yote na kudhibiti kwani awali wasindikaji wa ndani walikuwa wanakosa soko.

Amesema kuwa serikali inaendelea kuhakikisha uzalishaji na usindikaji wa maziwa unaongezeka ni  pamoja na mipaka yote,nchi zote zinzoingiza maziwa yote yaliyokuwa yanaingia bila kukaguliwa,bila kuchekiwa ubora wake,bila kulipiwa kodi na leseni yote mengine yameisha muda wake yanakamatwa 

AIDHA Mhe.Mpina ametoa maelekezo kwa bodi ya maziwa kwamba ifikapo julai 30 mwaka huu ihakikishe kuwa mwananchi yeyote yule atakayehitaji mtamba asikose na kama itakuwahaipo hapa nchini basi ni vyema ikaagizwa nje ya nchi.

Amewataka bodi hiyo kuhakikisha wanakaa na kujadili bei halali ya maziwa ikishindikana serikali itatoa bei elelevu kwani maziwa yapo wazalishaji wanatafuta soko kwaajili ya kuyauza maziwa yao.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro aliyemuwakilisha mkuu wa mkoa anesema kwa asilimia kubwa wakazi wa Arusha ni wafugaji amesema changamoto kubwa iliyopo ni ng'ombe wa asili waliopo wanatoa lita chache sana kulingana na idadi ya ng'ombe waliopo kwa sasa.

Amesema kuhusu swala la viwanda mkoa wa Arusha tayari una jumla ya viwanda 18 na vinaendelea kufanya kazi.
Nae msajili wa Bodi ya maziwa nbi Sophia Mbete amesema kuwa lenho kuu la maonyesho hayo ya maziwa na bidhaanzitokanazo na maziwa ni kubadikishana uzoefu na kujifunza mbinu zanuzalishaji maziwa na usindikaji kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini.

Amesema kuwa wameweza kupata washiriki 22 kutoka Iringa,Songwe,14 kati yao wanatoka mkoa wa Mbeya waliojitokeza kwaajili ya kuja kujifunza isindikaji wa maziwa,siagi,jibini na Mtindi.

Maadhimisho ya 22 ya wiki ya maziwa duniani ambayo yametanyika kitaifa mkoa wa Arusha yalizinduliwa rasmi na Katibu tawala wa mkoa wa Arusha Richard Kwitega na leo yamehitimishwa na Waziri wa Mifugo na Viwanda Luhaga Mpina ambapo wadau 46 wameahiriki pamoja na taasisi 4 za kifedha.

Share To:

Vukatz Blog

Post A Comment: