Mweyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya United Bank
for Africa, Tony Elumelu, akifurahia jambo na washiriki wengine kwenye sherehe
ya miaka 70 ya utoaji huduma kwa benki hiyo kwa nchi zaidi ya 50 za Afrika.
Sherehe hiyo ilifanyika hivi karibuni jijini
Lagos nchini Nigeria
LAGOS, NIGERIA
BENKI ya United Bank of
Africa (UBA) imeadhimisha miaka 70 tangu ianze kutoa huduma za kibenki kwa
wateja wake wakati wa sherehe zilizoongozwa na Mwenyekiti wa kundi la kampuni
Tony O. Elumelu.
Sherehe hizo
zilizohudhuriwa na wateja, wafanyakazi na marafiki pia zilienda sambamba na
hafla ya utoaji Tuzo za kila mwaka za Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO).
Tuzo hizo zilitolewa mbele
ya maelfu ya wageni kwa wafanyakazi wa UBA kutoka nchi zote 23 ambako
inaendesha shughuli zake kutokana na utendaji wao uliotukuka wa kipindi cha mwaka
mmoja uliopita.
Miongoni mwa watu
mashuhuhuri katika usiku huo pamoja na makadhi, magavana wa zamani na sasa wa
majimbo mbalimbali ya Nigeria.
Aidha marais wa zamani
Olusegun Obasanjo na Ibrahim Babaginda, ambao walishindwa kuhudhuria kutokana
na dharura walituma barua za kuipongeza benki hiyo kwa ufanisi na mafanikio makubwa
yaliyopatikana.
Mwenyekiti wa UBA Plc, Tony
Elumelu, ambaye aliambatana na mkewe Dk. Awele, alisema UBA imebakia kuwa
taasisi ya kifedha inayoongoza barani Afrika na kutimiza kwake miaka 70 ni
mafanikio makubwa.
Alisema, “Huu ni wakati wa kusherehekea urithi tajiri wa kipindi cha miaka mingi na kumwambia kila mtu aliyechangia kile kinachoifanya UBA isimame imara leo hii, kuwa tunashukuru kwa yote na jinsi walivyohakikisha uwekezaji uliowekwa katika benki kipindi cha miongo iliyopita unalipa.”
Shukrani kama hizo
zilitolewa pia na CEO wa Kundi la Kampuni, Kennedy Uzoka huku Mwenyekiti wa
Benki ya Zenith, Jim Ovia, akiisifu menejimeni na wafanyakazi wa UBA kwa
kuifikisha hapo ilipo.
Ovia alisema; “ UBA
inabakia kuwa moja ya benki kubwa kabisa Kusini mwa Sahara Afrika. UBA
imeanzishwa kwa ajili ya kudumu. Nawapongeza wafanyakazi wote na wanahisa.
Najuta kutonunua hisa za UBA, lakini nadhani sijachelewa kufanya hivyo.
Post A Comment: