Halmashauri ya Wilaya ya
Mbozi imetakiwa kubadilisha mahali pa kutupa takataka (dampo) kutoka eneo la
Ilembo lilipo sasa kwakuwa maji yanayotiririka kutoka katika eneo hilo yanaweza
kuelekea katika chanzo cha maji cha Mantengu ambacho kinatarajiwa kuanza
kutumika muda si mrefu.
Agizo hilo limetolewa na
Mkuu wa Mkoa wa Songwe Brig. Jen. (Mst) Nicodemus Mwangela wakati wa ziara yake
ya kukagua miradi ya maji iliyopo Wilayani humo.
Brig. Jen. (Mst) Mwangela
amesema zoezi la kubadilisha eneo lakutupa takataka lifanyike haraka kwakuwa
mradi wa Maji wa Vwawa ambao unatumia chanzo cha Maji cha Mantengu umekamilika
na hivi karibuni utaanza kuwafikia wananchi.
“Ile sehemu ya dampo
ibadilishwe, maji yameshaanza kutoka na yatawafikia wananchi hivi karibuni,
hivyo nawaagiza halmashauri utekelezaji wa hili ufanye haraka,”amesisitiza Brig.
Jen. (Mst) Mwangela
Ameongeza kuwa licha ya
kuwa eneo la kutupa takataka litabadilishwa lakini wahakikishe wanazoa takataka
zilizopo kwakuwa zikibaki pale zitaendelea kuchafua maji.
“Ili chanzo cha Mantengu
kibaki salama na maji yawe salama zile takataka zitolewe mara baada ya kuhamisha
dampo, licha ya kuwa tunafahamu kuna utaratibu wa kuyachuja na kuyawekea dawa
maji hayo bado kuna baadhi ya sumu haziwezi kumalizwa na madawa hayo”,
amefafanu Brig. Jen. (Mst) Mwangela
Kwa upande wake Mkuu wa
Wilaya ya Mbozi John Palingo amesema kuwa halmashauri ya Wilaya ya Mbozi
itatekeleza agizo hilo na sasa eneo la kutupa takataka litahamishiwa Mbozi
Mission ili kulinda chanzo hicho cha maji cha Mantengu.
Post A Comment: