Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma.
Serikali imesema kuwa halmashauri ambayo haina uwezo wa kujiendesha  kimapato ikiwa ni pamoja na uwezo wa kulipa posho za Madiwani haina sifa ya kuwa Halmashauri kwa mujibu wa     Sheria  na inapaswa kufutwa.
 
Hayo yamesemwa jana April 24,2019  bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais na Serikali Mitaa ,TAMISEMI,Mwita Waitara wakati akijibu swali la  Mbunge wa Mbulu Vijijini Mhe,Flatei Grigory Massay aliyehoji kwa baadhi ya halmashauri kushindwa kulipa posho za Madiwani ,je,serikali ina mpango gani wa kubadilisha mfumo wa kuwalipa posho Madiwani kupitia hazina kama watumishi wengine huku pia akihoji mpango  wa serikali kuanza kuwalipa posho Wenyeviti wa vijiji na mitaa kutokana na kazi kubwa wanayofanya.
 
Katika majibu yake Naibu Waziri wa TAMISEMI Mwita Waitara amesema halmashauri ambayo haina uwezo wa kujiendesha kimapato kwa mujibu wa Sheria inapaswa kufutwa na ametoa maelekezo kwa wakurugenzi kote nchini kuhakikisha wanalipa posho kwa madiwani huku akisema  kuwa kila asilimia 20 ya Mapato ya ndani ya halmashauri inatakiwa irejeshwe vijijini ama mitaani hali itakayowezesha kulipwa  wenyeviti wa mitaa na vijiji.

Hata hivyo Waitara amesema serikali inatambua kazi kubwa zinazofanywa na Madiwani ambapo mwaka 2012/2013  posho za madiwani zilipandishwa kutoka  Tsh.laki moja na nusu[1,50,000]   kwa mwezi hadi  Tsh.laki mbili na nusu [2,50,000]  kwa mwezi, kwa waraka wa mwaka 2012  sawa na ongezeko la asilimia 108.3%.
 
Mwaka 2014/2015 serikali ilipandisha posho za madiwani kupitia waraka wa mwaka 2014  kutoka  Tsh.laki mbili na nusu[2,50,000] hadi Tsh. laki tatu na nusu [3,50,000] kwa mwezi  sawa na ongezeko la asilimia arobaini[40%].
 
Vilevile Serikali inalipa posho ya madaraka kwa wenyeviti wa kamati  Tsh.elfu themanini[80,000] kwa mwezi  na posho ya kikao Tsh.elfu arobaini[40,000] kwa mujibu wa waraka wa mwaka 2007  na kigezo kinachotumika kupandisha posho za madiwani ni uwezo wa halmashauri kukusanya mapato.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: