Serikali kupitia Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(OR-TAMISEMI) imepata kibali Cha kuajiri jumla ya walimu 4549 Kati ya 91108 walio tuma maombi yao.

 Waziri wa Nchi OR-TAMISEMI, Seleman Jafo amesema kuwa Rais Dk.John Pombe Magufuli katika kuhakikisha Serikali inawahudumia vizuri wananchi ameamua kufungua dirisha la ajira kwa walimu.

Jafo alisema jumla ya waombaji 91108 waliojitokeza na kutuma maombi yao katika nafasi mbalimbali na kati ya hayo 43770 sawa na asilimia 48.04 yalikuwa na viambatanisho vyote vilivyohitajika.

Hata hivyo alieleza kuwa maombi 47338 sawa na asilimia 51.96 hayakuwa na vigezo ikiwa ni pamoja na kukosa viambatanisho muhimu vilivyohitajika.

==>>Tazama Hapo chini


Share To:

msumbanews

Post A Comment: