Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Ndugu Mzee Mkongea Ali (kushoto) akitoa pongezi kwa uongozi wa Mkoa wa Rukwa ukiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Mh. Joachim Wangabo (kulia) muda mfupi kabla ya Mwenge wa Uhuru kuelekea Mkoani Katavi tarehe 11.4.2019.
Mkuu wa Mko a wa Katavi Mh. Amos Makalla (kulia) akipokea Mwenge wa Uhuru kutoka kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kushoto) katika viwanja vya shule ya msingi Milumba Mkoani Katavi.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa siku tatu kwa wakuu wa wilaya wanaosimamia halmashauri ambazo Mwenge wa Uhuru umekataa kuweka mawe ya msingi au kuzindua miradi iliyopitiwa na Mwenge huo kutoa maelezezo ya kina juu ya sababu ya kukataliwa kwa miradi hiyo yenye tamani ya shilingi 1,248,489,871.
“Napenda nitoe maelekezo kwa Waheshimiwa Wakuu wa Wilaya wenye miradi iliyokataliwa kunipa taarifa ya kwanini miradi yao haikuzinduliwa/kuwekewa mawe ya msingi. Maelezo hayo niyapate ndani ya siku tatu kuanzia tarehe ya leo hadi tarehe 14, April, 2019,” Alisisitiza.
Ameyasema hayo muda mfupi kabla ya kukabidhi Mwenge wa Uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Katavi Mh. Amos Makalla huku Mwenge huo ukiwa umekimbizwa katika halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa zikichukua umbali wa kilemeta 832.5 na kutembelea miradi 35 na vikundi 11 ikiwa na tamani ya shilingi 45,404,104,489.59
Aidha, kutokana na mbio hizo za Mwenge wa Uhuru kubeba kauli mbiu isemayo “Maji ni haki ya Kila mtu, tutunze vyanzo vyake na tukumbuke kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa,” hivyo alitoa wito kwa wananachi kuendela kutunza vyanzo vya maji, kuimarisha jumuia za watumia maji pamoja na kufanya maandalizi thabiti ya kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa na kujitokeza kwa wingi katika uchaguzi huo.
Kwa upande wake Mkimbiza Mwenge wa Uhuru kwa Mwaka 2019 Ndugu Mzee Mkongea Ali aliushukuru uongozi wa Mkoa wa Rukwa kwa kumpa ushirikiano wa Kutosha tangu wanawasili katika mkoa huo hadi kuondoka na kuelekea katika mkoa wa Katavi na kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kwa kufikisha asilimia 55 ya wananchi wa Mkoa huo kupata maji safi na salam.
“Mimi nikupe hongera kwasababu takwimu zinaonyesha katika mkoa wako wa Rukwa umejitahidi kwa asilimia 55 kuhakikisha wananchi woyte wanapata maji ya uhakika na salama sambamba na hilo katika kupambana na Rushwa katika TAKUKURU kuna malalamiko 64 na kesi 59 wanazifanyia kazi, endeleeni kufanya kazi na kuhakikisha haki inapatikana kwa wote,” Alisema.
Kutokana na mapungufu yaliyobainika Mwenge wa Uhuru haukuzindua amakuweka mawe ya msingi kwenye miradi mitatu, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga mradi mmoja vyumba vitano vya madarasa wenye thamani ya shilingi 76,250,000, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga mradi mmoja wa ujenzi wa nyumba ya waalimu “6 in 1” wenye thamani ya shilingi 174,977,775 na Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo mradi mmoja wa maji wenye thamani ya shilingi 997,262,096.
Share To:

Post A Comment: