Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo, akibadilishana jambo na Mganga Mkuu wa mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe kwenye Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama
Baadhi ya washiriki na wadau wa Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama wakiwa katika uzinduzi huo
Mganga mkuu wa mkoa wa Arusha Dkt. Wedson Sichalwe akizungumza. Katika Uzinduzi wa Kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama.


Na.Vero Ignatus,Arusha.

Uzinduzi wa kampeni ya jiongeze tuwavushe salama umefanyika mkoani Arusha ikiwa na lengo la ''Kupunguza vifo vitokananvyo na uzazi'' na  kuhakikisha mama na mtoto wanakuwa salama kabla na baada ya kujifungua. 

Akizungumza katika uzinduzi huo mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa watendaji wote wa wizara ya afya ngazi ya mkoa watende kazi kwa weledi ili waweze kupunguza vifo vya wakina mama wakati wa kujifungua ambapo kwa ngazi ya mkoa ni 40%na Kitaifa ni 28%

Kampeni hiyo iliyobeba Kauli mbiu isemayo''Jiongeze Tuwavushe Salama''na Maudhui yasemayo '' Kila mmoja wetu anao wajibu wa kuzuia vifo vitokanavyo na uzazi, maneno basi, sasa vitendo''

Amesema kuwa kampeni hiyo ni ya muhimu kwani inakwenda sambamba na lishe kwa mama mjamzito ili aweze kujifungua salama na mtoto atakayezaliwa awe mwenye afya njema

''Mwanaume ni wajibu wako kutambua kuwa mwanamke anapokuwa mjamzito ndio wakati wako wa kuwa karibu na mkeo, msindikize Kliniki, pimeni afya pamoja leeni mimba pamoja na mtoto akizaliwa mtamfurahia''. Alisema Gambo. 

Ameainisha sababu kuu ambazo zinasababisha vifo kwa akina mama wajawazito ni pamoja na mama kutohudhuria kliniki mapema,kutokwa damu nyingi  wakati wa kujifungua na baada ,shinikizo la damu.

Amesema lishe duni imekuwa sababu kubwa ya wakina  mama kujifungua watoto njiti ambapo pia vifo vya watoto hao ni 25 kati ya kila vizazi hai 1000husababishwa na kushindwa kupumua na wengine kuzaliwa kabla ya wakati.

Kwa upande wake Daktari mkuu wa mkoa Wedson Sichalwe amesema Tafiti zilizofanyika mwaka 2015/2016 zinaonyesha  kiwango cha vifo vitokanavyo na uzazi ni 556 kwa kila vizazi hai 100,000 ambayo ni sawa na vifo 11,000 kila mwaka,sawa na wanawake 30 hufariki kila siku, kutokana na matatizo yatokanayo na uzazi. 

Dkt. Sichalwe ameainisha kuwa changamoto kubwa waliyonayo  ni ukosefu wa dawa lishe,ukosefu wa virutubisho ambavyo hupelekea matatizo kwa mtoto akiwa tumboni hata kuzaliwa njiti au akiwa amefariki

Dkt amesema hiyo changamoto ya lishe katika mkoa imesababisha watoto wengine kuzaliwa wakiwa na udumavu halo inayopelekewa kuja  kuwa na taifa lenye watoto wengi wenye tatizo hilo endapo hatua za haraka hazitachikiliwa.

Baadhi ya washiriki na wadau wa afya akiwemo Dkt. Emmanuel Maeda amesema swala la elimu kwa jamii ni changamoto hivyo wao wamekuja na kitu kiitwacho Vunja ukimya kwaajili ya kumkumbusha mwanaume kutambua wajibu wake pale mke anapokuwa mjamzito. 

'' Mwanamke anapokuwa mjamzito inamuhitaji mwanaume kuelewa, anapaswa atambue mama mjamzito anahitaji lishe bora ili ajifungue salama, ikiwa kwenda pamoja kliniki na kutambua changamoto anazopitia na siyo wao kukaa pembeni na kusema kwani mimi ndo nimebeba mimba''alisema Dkt. Maeda. 

Nae Munga kutoka Japayco nae alishauri kuwa kuwepo na siku ya afya vijijini ina lazima juhudi ziongezwe kuhakikisha kuangalia zaidi  mama na kichanga anavuka salama na kila mjamzito lazima aende kliniki na hospitali kujifungua. 

Kampeni ya Jiongeze tuwavushe salama ilizinduliwa rasmi na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan  6Novemba 2018 mkoani Dodoma. 

Kampeni ya Jiongeze Tuwavushe Salama  inatekelezwa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto pamoja na Mashirika yasiyo ya kiserikali ikiwemo UNICEF.


Share To:

Post A Comment: