Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Peter Tino leo akikamilisha kufungua akaunti ili aweke shilingi Milioni 5 alizopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutambua mchango wake kwa Timu ya Taifa ya mwaka 1980 ambapo goli lake liliiwezesha Tanzania kufuzu fainali ya
Michuano ya Soka Barani Afrika (AFCON). Wanaoshuhudia ni Meneja Biashara wa Tawi la CRDB la Azikiwe, Bw. George Yatera na Afisa kutoka  TFF Bw. John Michael Mashaka. Kushoto ni Afisa wa Benki hiyo
Bi. Gloria Kaale ambaye ndiye aliyemfungulia akaunti nyota huyo wa zamani
Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Peter Tino akielekezwa  na Meneja Biashara wa Tawi la CRDB la Azikiwe, Bw. George Yatera  namna na kutumia kadi yake ya ATM  baada ya kukamilisha kufungua akaunti ili aweke shilingi Milioni 5 alizopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli
kwa kutambua mchango wake kwa Timu ya Taifa ya mwaka 1980 ambapo goli lake liliiwezesha kufuzu fainali ya Michuano ya Soka Barani Afrika (AFCON).  Kushoto ni Afisa wa Benki hiyo Bi. Gloria Kaale
Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars)Peter Tino akikabidhiwa kadi yake ya ATM kutoka kwa  Meneja Biashara wa Tawi la CRDB la Azikiwe, Bw. George Yatera  baada ya kukamilisha kufungua akaunti ili aweke shilingi Milioni 5 alizopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa
kutambua mchango wake kwa Timu ya Taifa ya mwaka 1980 ambapo goli lake liliiwezesha kufuzu fainali ya Michuano ya Soka Barani Afrika (AFCON).  Wanaoshihudia ni Afisa kutoka kutoka  TFF Bw. John Michael Mashaka
na Afisa wa Benki hiyo Bi. Gloria Kaale ambaye ndiye
Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Peter Tino akionesha kadi yake ya ATM  baada ya kukamilisha kufungua akaunti ili aweke shilingi Milioni 5 alizopewa na Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutambua mchango wake kwa Timu ya Taifa ya mwaka 1980 ambapo goli lake liliiwezesha kufuzu fainali ya Michuano ya Soka Barani Afrika (AFCON).
Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Peter Tino akimshukuru  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kumzawadia  shilingi Milioni 5  kwa kutambua mchango wake kwa Timu ya Taifa ya mwaka 1980 ambapo goli lake
liliiwezesha Tanzania kufuzu fainali ya Michuano ya Soka Barani Afrika (AFCON) wakati Rais Magufuli alipokutana na kuwapongeza wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ambao jana waliifunga Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) na kufanikiwa kufuzu kucheza fainali za
AFCON 2019 zitakazofanyika baadaye mwezi Juni 2019 huko Misri.

Na Sultani Kipingo

Mchezaji wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) Peter Tino leo amekabidhiwa shilingi Milioni 5 alizopewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutambua mchango wake kwa Timu ya Taifa ya mwaka 1980 ambayo ilifuzu kuingia
fainali Michuano ya Soka Barani Afrika (AFCON).

Mchezaji Peter Tino ndiye aliyefunga goli lililoiwezesha Tanzania kuingia fainali hizo  na tangu mwaka huo wa 1980 Tanzania haikuwahi kufanikiwa tena kuingia hatua hiyo mpaka mwaka 2019 ikiwa ni miaka 39imepita.
 
 Peter Tino alialikwa Ikulu Jijini Dar es Salaam leo tarehe 25 Machi, 2019 wakati Mhe. Rais Magufuli alipokutana na kuwapongeza wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) ambao jana waliifunga Timu ya Taifa ya Uganda (The Cranes) na kufanikiwa kufuzu kucheza fainali za
AFCON 2019 zitakazofanyika baadaye mwezi Juni 2019 huko Misri.

 Pamoja na kupatiwa shilingi Milioni 5, Peter Tino pia ameunganishwa katika zawadi ya kupatiwa kiwanja Jijini Dodoma kwa kila mchezaji wa Taifa Stars iliyotolewa na Mhe. Rais Magufuli ambapo naye atapatiwa kiwanja cha kujenga nyumba.

 Peter Tino amezeweka pesa hizo katika akaunti yake ya Benki ya CRDB aliyoifungua mara tu baada ya kutoka Ikulu na kukabidhiwa kadi yenye taarifa zake za benki (ATM).

“Hakika Mungu ni mkubwa” amesema Peter Tino baada ya kupokea kadi yake ya Benki kwa Meneja Biashara wa Tawi la CRDB la Azikiwe, Bw. George Yatera, akishuhudiwa na Afisa kutoka kutoka  TFF Bw. John MichaelMashaka.

 “Hela hii sikuiota hata ndotoni na mradi Raisi wetu mpendwa John Pombe Magufuli kanikumbuka hakika sintomwangusha. Yaani nitakwenda kumalizia kibanda changu kule Morogoro, ” aliongezea.

Afisa wa Benki hiyo Bi. Gloria Kaale ndiye aliyemsajili mchezaji huyo ambaye wadogo zake, Gebbo Peter na Emma Peter, nao walitikisa anga za soka nchini kwa nyakati tofauti siku za nyuma kabla ya na wao kustaafu. Familia yao kwa sasa inaishi Morogoro.


Kwa mujibu wa kumbukumbu zilizopo, ilikuwa ni Agosti 26,1979 wakati timu ya soka ya Taifa, Taifa Stars ilipokuwa ikirudiana na timu ya soka ya Taifa ya Zambia katika mechi ya michuano ya kuwania kufuzu kucheza fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika za mwaka 1980
zilizofanyika nchini Nigeria.Pambano hilo lilichezwa mjini Ndola.


Mechi hiyo ilikuwa na umuhimu mkubwa kwa Taifa Stars kwa vile ilikuwa ikihitaji sare ya aina yeyote ili iweke historia ya kufuzu kucheza fainali hizo kwa mara ya kwanza , tangu ilipoanza kushiriki michuano hiyo mwaka 1968. Katika mechi ya kwanza iliyochezwa wiki mbili nyuma
kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Taifa Stars iliishinda Zambia bao 1-0. Bao hilo lilifungwa na kiungo Mohammed Rishard Adolph.

Ushindi huo ulipatikana kwa mbinde kiasi kwamba mashabiki wengi hawakuwa na imani iwapo Taifa Stars ingeshinda ama kupata sare katika mechi ya marudiano. Na hivyo ndivyo ilivyokuwa kwani Wazambia walifanikiwa kupata bao la kuongoza dakika za mapema na kudumu nalo
kwa takriban dakika 86.

Zikiwa zimesalia dakika tatu pambano hilo kumalizika, mshambuliaji mrefu mwenye kasi na mashuti makali, Peter Tino alibadili sura ya mchezo na kufanya kile kilichokuwa kikisubiriwa kwa hamu kubwa na mashabiki wa mchezo huo nchini.

Ilipigwa kona kwenye lango la Taifa Stars, kipa Juma Pondamali akaupangua mpira kwa ngumi, ukamkuta kiungo Leodegar Tenga, aliyetoa pasi ndefu kwa kiungo mwenzake, Hussein Ngulungu, ambaye naye alitoa pasi ndefu kwa Tino.

Akiwa amezungukwa na mabeki watatu wa Zambia, Tino alilazimika kupiga hesabu za haraka haraka. Aliwachomoka mbio mabeki nao na kukimbia na mpira kwa kasi. Alipofika nje kidogo ya eneo la hatari la Zambia, alifumua shuti kali la mguu wa kulia, lililompita kipa Shileshi wa
Zambia na mpira kutinga wavuni.Bao hilo lilipatikana baada ya pasitatu.

Katika mechi hiyo, Taifa Stars iliwakilishwa na kipa Juma Pondamali,mabeki ni Leopard Tasso, Mohammed Kajole/ Ahmed Amasha, Salim Amir, Jella Mtagwa, viungo ni Leodegar Tenga, Hussein Ngulungu na washambulaji ni Omari Hussein, Peter Tino, Mohamed Salim na Thuweni
Ally.

Kikosi hicho kilikuwa chini ya Kocha Slowmir Work kutoka Poland, akisaidiwa na Wazawa Joel Bendera na Ray Gama (ambao kwa sasa wote ni marehemu), ndicho kilichoiwakilisha Tanzania katika fainali za kombe hilo zilizofanyika nchini Nigeria.

Katika fainali hizo, Taifa Stars ilichapwa mabao 3-1 na wenyeji Nigeria katika mechi ya ufunguzi, ilitoka sare ya mabao 2-2 na Ivory Coast kabla ya kuchapwa mabao 2-1 na Misri na kutolewa hatua ya makundi.

Hiyo ilikuwa ni miaka 39 iliyopita ambapo hivi sasa, baada ya kuichapa Uganda mabao 3-0 Jumapili, kila Mtanzania ameweka matumaini kwenye kikosi hicho kipya kilicho chini ya kocha kutoka Nigeria, EmmanuelAmunike.

Mwisho
Share To:

Post A Comment: